https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

/ 7

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

tutachunguza dhana ya maskini na utume kupitia dhana tajiri ya kibiblia ya “shalom , ” au ukamilifu. Kama jamii ya agano ya Yehova, watu wa Israeli waliitwa kuishi kwa uaminifu katika agano la Bwana kwa kiwango ambacho kingesababisha umaskini uondolewe kupitia matendo ya haki na uadilifu. Akijenga juu ya tendo la ukombozi wake kwa watu wake kutoka Misri wakati wa tukio la Kutoka, Mungu aliwapa watu wake katika agano lake ramani ya mfumo wa haki ambao ungeshughulikia suala la umaskini na uonevu. Tukiwa na mtazamo huo wa Biblia, tutachunguza jinsi Yesu kama Masihi na Kichwa cha Kanisa anavyotimiza unabii wa Kimasihi kuhusu Yule ambaye angeleta haki na amani kwa maskini. Yesu kama Bwana na Kichwa cha Kanisa anaendelea kudhihirisha agizo la Mungu kwa ajili ya shalom kati ya watu wa Mungu, na kupitia watu wake, shalom ienee ulimwenguni. Kanisa, jamii ya agano jipya la Mungu kwa imani katika Yesu, limeitwa kuishi katika shalom na kuwaonyesha washirika wake na ulimwengu kwa ujumla haki ya Mungu kwa waliovunjika moyo. Hili linawezekana sasa kwa sababu ya Roho Mtakatifu anayewatia nguvu na kuwawezesha watu wa Mungu leo. Kama waaminio katika Yesu Kristo, kila mmoja wetu, kila kusanyiko limekombolewa ili tuweze kuwa watu wa ukombozi, kutangaza na kuiishi kweli ya Mungu pale alipotuweka. Kwa kweli, kuwa Mkristo ni kuwa na mwelekeo wa utume na kutengenezwa kwa ajili ya utume; tulizaliwa kutoka juu ili tuwe watenda kazi pamoja na Mungu katika utume wake wa kuvuna ulimwengu kwa ajili ya Mwanawe (Mdo. 9:15). Mungu na atumie kozi hii kukupa changamoto ya kufanya sehemu yako katika hadithi hii ya ajabu ya utukufu wa Mungu, na umisheni wake wa kuuleta ulimwengu kwake kwa njia ya Mwanawe na Mwokozi wetu, Yesu Kristo! - Mchungaji Dr. Don L. Davis

Made with FlippingBook Annual report maker