https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

6 /

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

kupitia utume wa kutangaza Injili, ahadi ya maisha mapya inatolewa kwa mataifa kupitia kuhubiriwa kwa Neno la msalaba. Katika somo la pili, Maono na Msingi wa Kibiblia wa Utume wa Kikristo (2) , tutachunguza utume kama Mapenzi ya Enzi na kama Vita vya Milki . Taswira hizi katika Maandiko zinatusaidia kuona jinsi utume ulivyo muhimu kwa theolojia yetu kama waamini. Kama Mapenzi ya Kiungu, tunaona azimio la Mungu la kuwatoa ulimwenguni watu ili wapate kuwa milki yake mwenyewe. Tutapitia mada hii muhimu, tukianza na historia ya Israeli kama mke wa Mungu, na taifa hilo lilivyokosa uaminifu kwa kugeukia ibada ya sanamu na kutotii. Tutafuatilia mada hii katika utu wa Yesu, na kuona jinsi agano jipya lilivyopanua wigo wa dhana ya “watu wa Mungu” ili kuwajumuisha Mataifa. Kama Vita vya Milki, tunaona tangazo la utawala wa ufalme wa Mungu kwa njia ya Yesu wa Nazareti. Tukianzia na uthibitisho wa wazi wa ukuu wa Mungu, tunaona kwamba Mungu ameamua kuweka upya utawala wake juu ya uumbaji wake, ambao ulianguka kutoka katika neema yake kupitia uasi wa shetani na wanadamu wakati wa Anguko. Tangu wakati huo, Mungu amechukua nafasi ya Shujaa ili kuurudisha ulimwengu chini ya utawala wake. Kwa njia ya Yesu wa Nazareti, Mungu anathibitisha tena haki yake ya kutawala ulimwengu mzima, na umisheni ni kutangaza ujio wa Ufalme huo kwa nji ya Kristo Yesu. Katika somo la tatu, Utume wa Kikristo na Jiji , tunaelekeza mawazo yetu kwenye lengo la utume na nia ya Mungu kwa ajili ya miji na watu maskini. Tunaanza kwa kuutazama mji wa kale, mpangilio wake na sifa zake, hasa sifa yake kama ishara ya uasi dhidi ya Bwana. Tutazingatia umuhimu wa kiroho wa jiji, tukiangalia namna Mungu alivyoshughulika na miji kadha wa kadha katika Maandiko, na kuchunguza maana ya mambo hayo. Tutaona jinsi ambavyo Mungu ameikubali dhana ya mji kwa makusudi yake mwenyewe, akibatilisha uhusiano kati ya dhana ya mji na uasi na ibada ya sanamu, na kuikomboa maana na msingi wa dhana hiyo kwa ajili ya utume, na kwa ajili ya utukufu wa Ufalme ujao. Hivyo, katika somo hili tutatoa mantiki ya kuhusika kwetu katika umisheni wa mijini. Jiji ni makao ya ushawishi, mamlaka, na shughuli za kiroho na vilevile sumaku inayowavuta walioonewa, waliovunjika moyo, na maskini. Kwa sababu hiyo, sisi kama wanafunzi wa Kristo katika karne ya 21, lazima tujitahidi kutamka matamko ya kinabii juu ya jiji na kuishi kinabii ndani ya jiji. Kama picha na ishara ya hatima na urithi wetu wa kiroho, lazima tufanye yote tuwezayo kuinjilisha watu, kufuasa watu (yaani kufanya watu kuwa wanafunzi wa Kristo), na kupanda makanisa katika miji yetu, ndani na nje ya nchi. Hatimaye, katika somo la nne tunachunguza kipengele kingine muhimu cha utume wa Kikristo. Katika somo hili liitwalo Utume wa Kikristo na Maskini ,

Made with FlippingBook Annual report maker