https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

/ 5

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

Utangulizi wa Moduli

Salamu, katika jina lenye nguvu la Yesu Kristo! Mada ya utume (umisheni) haijapewa mkazo na uzingativu upasao katika makanisa yetu ya mijini. Baada ya kuonekana kwa kiasi kikubwa kama kazi ya kuvuka bahari kwenda pembe za mbali za dunia, tumeshindwa kuipa uchambuzi wa kina na muhimu ambao inastahili. Kwa mtazamo wa upande mmoja, ukamilifu wa imani ya Kikristo unaweza kuonekana kama mwitikio wa utume, wito wa kwenda kwa mataifa na kumtangaza Yesu wa Nazareti kama Bwana na Mfalme wa utawala wa Mungu. Agano Jipya ni mkusanyo wa hati za kimishenari zilizotolewa kwa makanisa ambayo yalianzishwa na mitume, wamishenari wa awali wa imani ya Kikristo. Mungu mwenyewe ndiye mmishenari wa asili, aliyekuja ulimwenguni kwa njia ya Kristo na kuupatanisha ulimwengu na nafsi yake (2Kor. 5:18-21). Hakika, Ukristo ni utume. Kwa hiyo, moduli hii inashughulikia mada hii muhimu kwa nia ya kukusaidia wewe, kiongozi wa watu wa Mungu unayeandaliwa jijini, kuelewa theolojia ya utume na matokeo ya utume katika mtazamo wa kibiblia. Kwa maana halisi, hatuwezi kuelewa kile ambacho Mungu anafanya ulimwenguni kupitia utume bila kuwa na picha au muhtasari wa maono ya kusudi la Mungu na kazi yake. Kwa hiyo, katika masomo yetu mawili ya kwanza tutaangalia utume kupitia mitazamo minne tofauti: utume kama tamthilia na ahadi, na utume kama mapenzi na vita mtawalia. Katika somo letu la kwanza, Maono na Msingi wa Kibiblia wa Utume wa Kikristo (1) , tunashughulikia mtazamo wa utume (umisheni) kama Tamthilia ya Nyakati Zote. Nia yetu hapa ni kutoa mfumo wa kuielewa kazi ya utume kwa msingi wa Maandiko yenyewe. Tutaanza kwa kutoa ufafanuzi wa jumla wa utume, na kisha kuelezea muhtasari wa haraka wa vipengele muhimu vya ufahamu wa kibiblia wa utume. Tutaangalia utume kupitia mtazamo wa hadithi na tamthilia, tukionyesha kupitia Maandiko kwamba utume ni mamlaka kuu ya Mungu inayofanya kazi kupitia historia katika enzi au vipindi mbalimbali vya wakati ili kuleta ukombozi kwa njia ya Kristo. Pia tunaangazia utume kama utimilifu wa ahadi ya Mungu, tukiutazama utume kama utendaji wa Mungu katika kutimiza ahadi yake kama Mungu mwaminifu wa agano. Tutaelezea jukumu la maagano ya kibiblia katika Maandiko, na kufuatilia utendaji wa Mungu kama mwitikio wake kwa ahadi yake ya agano kwa Ibrahimu, iliyothibitishwa katika wanawe na mababa wa Taifa la Israeli, iliyohusishwa na kabila la Yuda na kufafanuliwa katika ahadi ya Mungu kwa Daudi ya kuwa na mrithi wa milele kwenye kiti chake cha enzi. Katika nafsi ya Yesu wa Nazareti, ahadi iliyotolewa kwa Ibrahimu na Daudi imetimizwa, na sasa,

Made with FlippingBook Annual report maker