https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

1 8 /

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

• Kuelezea kukamilishwa kwa awamu za kusudi la Mungu linaloendelea kujifunua kuelekea Utimilifu wa Wakati (ambao ni pamoja na Kristo kuvaa mwili, kufunuliwa kwa Ufalme katika Yesu, mateso, kifo, ufufuo, na kupaa kwa Kristo); Nyakati za Mwisho (ni pamoja na kushuka kwa Roho Mtakatifu, kuanzishwa kwa Kanisa, kujumuishwa kwa Mataifa, na enzi ya utume wa ulimwengu), awamu ya Ukamilifu wa Wakati (ambayo inahusisha mwisho wa uinjilishaji wa ulimwengu, uasi wa Kanisa, Dhiki Kuu, Parousia , utawala wa Kristo duniani, Kiti Kikubwa cha Enzi Cheupe, Ziwa la Moto, na Kristo kukabidhi Ufalme kwa Mungu Baba), na hatimaye awamu ya Baada ya Wakati (ambayo inajumuisha mbingu mpya na nchi mpya, kushuka kwa Yerusalemu Mpya, nyakati za kuburudishwa, na kuingizwa kwa Enzi Ijayo). • Kufanya muhtasari wa maana za Utume kama Tamthilia ya Nyakati Zote : jinsi kusudi kuu la Mungu linavyoweka msingi wa historia yote ya mwanadamu, Mungu kama mhusika mkuu katika awamu za tamthilia ya kiungu zinazoendelea kujifunua, utume kama kurejesha kile kilichopotea mwanzoni mwa wakati, na kazi ya kufanya mataifa wote kuwa wanafunzi kama sehemu yetu katika kutimiza jukumu letu katika muswada (script) wa Mwenyezi Mungu . • Kutoa muhtasari wa vipengele vikuu vya Utume kama utimilifu wa ahadi ya Mungu, kwa kuanzia na ufafanuzi wa agano kama mkataba kati ya pande mbili, iwe watu binafsi, makabila, au mataifa; pamoja na kuwa na wajibu wa kutimiza masharti ya mkataba huo, na faida na manufaa kama matokeo ya kutimizwa kwa masharti hayo. • Kuelezea sifa kuu za kufanya agano katika Maandiko ikijumuisha jinsi walivyoitishwa na shahidi, walivyokuwa makini (yaani, kuvunja masharti ya mkataba kulionekana kama uovu mkubwa wa kimaadili), mkataba ulivyotolewa ushahidi kwa kutoa zawadi, kula chakula, na kuweka mawe ya ukumbusho, na ulivyothibitishwa kwa kiapo na kwa dhabihu. • Kutoa mifano kadhaa ya maagano katika Biblia, ikijumuisha agano la ndoa, agano na Nuhu, agano la Sinai na wana wa Israeli, ambayo yote yanazungumzia mkataba mzito kati ya watu binafsi, au kati ya Mungu na watu. • Kuchunguza taswira ya utume kama utimilifu wa ahadi ya Mungu iliyotolewa katika agano kati ya Mungu na Ibrahimu, pamoja na sharti lake la kwamba aondoke kutoka katika nchi yake na jamaa yake na kwenda katika nchi aliyoichagua Mungu mwenyewe, pamoja na baraka inayoambatana na

1

Made with FlippingBook Annual report maker