https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

/ 1 9

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

sharti hilo kwamba Mungu angemfanya kuwa taifa kubwa, angembariki na kulikuza jina lake, kuwabariki wambarikio na kuwalaani wamlaanio, na kuzibariki jamaa zote za dunia kupitia yeye. • Kuangazia jinsi agano hilo la Abrahamu lilivyohuishwa, likathibitishwa kupitia Isaka na Yakobo, na kuhusishwa na Yuda kuwa kabila ambalo Masihi wa Mungu angetokea, na kuonyesha jinsi Uzao wa kifalme ulioahidiwa katika baraka za Abrahamu ungekuja kupitia agano la Mungu na Daudi na nyumba yake, ambaye mrithi wake angetawala milele juu ya nyumba ya Israeli na kuwa baraka kwa mataifa. • Kuonyesha jinsi ahadi hii ilivyotimizwa katika Yesu wa Nazareti, ambaye anawakilisha mfano halisi wa ahadi zilizotolewa kwa Ibrahimu na Daudi. Kupitia maisha yake, kifo, ufufuo, na kupaa kwake, ahadi ya agano ya Mungu imetimizwa. • Kueleza namna ambavyo utume ni kutangazwa kwa Habari Njema kuhusu uaminifu wa agano la Mungu, na Agizo Kuu kama jukumu la kutangaza ahadi iliyotimizwa kwa ajili ya wokovu wa wanadamu wote, kuanzia Yerusalemu, hadi miisho ya dunia. • Kuonyesha uhusiano uliopo kati ya jukumu la utume katika enzi hii na tamko la kwamba katika Yesu wa Nazareti ahadi iliyotolewa kwa Ibrahimu na Daudi imetimizwa, na sasa, kupitia utume wa kutangaza Injili, ahadi ya maisha mapya inatolewa kwa mataifa kupitia kuhubiriwa kwa Neno la msalaba. Rum. 16:25-27- Sasa na atukuzwe yeye awezaye kuwafanya imara, sawasawa na injili yangu na kwa kuhubiriwa kwake Yesu Kristo, sawasawa na ufunuo wa ile siri iliyositirika tangu zamani za milele, 26 ikadhihirishwa wakati huu kwa maandiko ya manabii, ikajulikana na mataifa yote kama alivyoamuru Mungu wa milele, ili waitii Imani. 27 Ndiye Mungu mwenye hekima peke yake. Utukufu una yeye kwa Yesu Kristo, milele na milele. Amina. Labda hakuna kitu kinachovuta umakini kama vile misemo: “Hapo zamani za kale,” na ule unaoambatana nao kwa karibu: “Na wakaishi kwa furaha milele.” Tumepata kuisikia misemo hii – inawakilisha mwanzo na mwisho wa simulizi za hadithi, hekaya au ngano, hadithi ambazo wengi wetu tumezisikia tulipokuwa tukikua. Kusikia tu msemo “Hapo zamani za kale” kulitosha kabisa kutufanya “Kila wakati ni wakati wa hadithi” Hadithi ya Utukufu wa Mungu na Wito wa Utume

1

Ibada

Made with FlippingBook Annual report maker