https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi
/ 2 7 1
MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO
Nafasi ya Wanawake katika Huduma (muendelezo)
Bwana anamwita kutumika. Wanawake wangezuiwa kushika nafasi za uongozi kwa sababu Roho Mtakatifu hangeweza kumpa mwanamke wito huo na karama zinazohitajika kuutimiza kwa sababu tu ni mwanamke. Baadhi ya karama na vipawa vingekuwa maalum kwa ajili ya wanaume tu, na wanawake hawangepokea karama na vipawa hivyo. Usomaji makini wa maandiko haya na mengine yanayohusiana na mada hii hauonyeshi katazo kama hilo. Inaonekana kwamba ni juu ya Roho Mtakatifu kumpa mtu ye yote, mwanamume au mwanamke, kipawa chochote kinachomfaa kwa huduma yoyote anayotaka aifanye, kama apendavyo yeye (1Kor. 12:11, “lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye”). Akijenga juu ya jambo hili, Terry Cornett ameandika insha nzuri ya kitheolojia inayoonyesha jinsi neno la Kiyunani la AJ linalotafsiriwa kwa neno “mtume” linavyotumika kwa wanawake bila shaka, linaloonyeshwa kwa uwazi zaidi katika utoaji wa nomino ya kike, “ Junia ” inayotumiwa kuhusiana na “mtume” katika Warumi 16:7, pamoja na dokezo la kufanya kazi pamoja, kwa mfano, kwa habari ya mapacha Trifena na Trifosa, ambao “walifanya kazi” pamoja na Paulo katika Bwana (16:12). Tukiamini kwamba kila Mkristo aliyeitwa na Mungu, aliyekirimiwa na Kristo, aliyepewa vipawa na Roho na anayeongozwa naye anapaswa kutimiza wajibu wake katika Mwili, tunathibitisha wajibu wa wanawake kuongoza na kufundisha chini ya mamlaka ya kimungu inayonyenyekea kwa Roho Mtakatifu, Neno la Mungu, na yenye msingi katika mapokeo ya Kanisa na ufahamu thabiti wa kiroho. Tunapaswa kutarajia Mungu kuwapa wanawake karama za neema zisizo za kawaida ili kutekeleza agizo lake kwa niaba ya Kanisa lake, na utawala wake katika Ufalme wa Mungu. Kwa kuwa wanaume na wanawake wote wanaakisi Imago Dei (yaani, mfano wa Mungu), na wote wawili wanasimama wakiwa warithi pamoja wa neema ya Mungu (rej. Mwa. 1:27; 5.2; Mt. 19:4; Gal. 3:28; 1 Pet. 3:7), wao pia wamepewa fursa ya hadhi ya juu ya kumwakilisha Kristo pamoja kama mabalozi wake (2Kor. 5:20), na kupitia ushirikiano wao ili kukamilisha utii wetu kwa Agizo Kuu la Kristo la kuwafanya mataifa yote kuwa wanafunzi (Mt. 28:18-20).
Made with FlippingBook Annual report maker