https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

/ 2 5

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

sasa ni mada za matangazo ya redio ya usiku wa manane. Inaonekana leo kwamba ni watu wachache sana wenye tabia ya kutimiza ahadi au kuthamini nguvu ya ahadi iliyoiweka. Hata hivyo, hadithi nzima ya imani ya Kikristo ina mizizi katika uwezo wa kutambua jinsi ahadi ya Mungu kwa habari ya Mwokozi ilivyokuwa muhimu, na jinsi ahadi hiyo ilivyotimizwa kupitia Yesu wa Nazareti. Je, mmomonyoko huu wa uadilifu katika utoaji na utimizaji wa ahadi katika jamii yetu unaathiri vipi uwezo wetu wa kuelewa asili ya imani ya Kikristo, na pia kufanya huduma na utume katika jamii kama yetu? Je, unafikiri kwamba ukosefu wa uadilifu katika jamii yetu unaathiri uwezo wetu wa kuelewa na kuthamini uadilifu wa Mungu katika Injili, yaani wokovu ambao ametupatia katika Kristo? Eleza.

1

Maono na Msingi wa Kibiblia wa Utume wa Kikristo: Sehemu ya Kwanza Sehemu ya 1: Utume kama Tamthilia ya Nyakati Zote

YALIYOMO

Mchungaji Dkt. Don L. Davis

Utume ni tangazo la fursa ya wokovu na ukombozi wa Mungu kwa njia ya Yesu Kristo na kazi yake katika uwezo wa Roho Mtakatifu kwa makundi yote ya watu . Ukitazamwa kama tamthilia na hadithi ya Mungu, kutoka Kabla ya Wakati hadi Baada ya Wakati , tunaweza kuanza kuona jinsi ambavyo katika hadithi ya utume, Mungu wa Utatu anatenda kazi kama Mungu Mwenye Enzi Kuu , akitenda kazi katika mambo yote kwa utukufu wake na manufaa yetu. Lengo letu katika sehemu hii, Utume kama Tamthilia ya Nyakati Zote , ni kukuwezesha kuona kwamba: • Neno “ prolegomena ” linamaanisha “neno la kwanza,” na p rolegomena juu ya utume lazima ianze na mtazamo wa kibiblia wa ulimwengu juu ya Mungu na kazi yake duniani kupitia Yesu wa Nazareti. • Utume unaweza kufafanuliwa kama “tangazo la fursa ya wokovu na ukombozi wa Mungu kwa njia ya Yesu Kristo na kazi yake katika uwezo wa Roho Mtakatifu kwa makundi yote ya watu.” • Uelewa wa kibiblia wa utume una vipengele fulani ambavyo vinaweza kubainishwa kutokana na usomaji wa Maandiko yenyewe. Utume lazima ujengwe juu ya msingi wa ufahamu sahihi wa Mungu na makusudi yake kwa ulimwengu, kuhusianisha maelezo yote ya kihistoria katika mada moja. Mtazamo wa kibiblia wa utume, pia, lazima ujikite katika Maandiko

Muhtasari wa Sehemu ya Kwanza

Made with FlippingBook Annual report maker