https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi
2 4 /
MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO
na mashaka, halika linakuwa jambo gumu kuuchukulia ufufuo kama ukiri wenye ukweli ndani yake. Kwa nini unafikiri ni muhimu kwa kazi ya umisheni kila mara kuanza na ufahamu wa kihistoria wa imani ya Kikristo kabla ya kuanza kuzungumza juu ya kipengele cha umisheni cha kuwashirikisha wengine imani hiyo? Kwa nini maoni ya Paulo kuhusu ufufuo kama msingi wa mahubiri na mafundisho yote ya kweli kuhusu Kristo hayaruhusu wala kutoa nafasi kwa maoni yoyote ya Ukristo ambayo yanakataa kukumbatia thamani ya ukweli wa kihistoria wa hadithi na Injili yetu? Wakati ambapo Hollywood inalipuka kwa filamu za hekaya na hadithi nzito nzito ( Gladiator, The Lord of the Rings, The Chronicles of Narnia , n.k.) mimbari nyingi za Kikristo zimesalia zikiwa zimefungwa kwenye muundo wa kutunga hotuba na uwasilishaji wa mahubiri katika mfumo wa «vipengele vitatu, shairi, na maombi.» Aina hii ya mahubiri na uwasilishaji inaonekana kupuuza nguvu ya hadithi katika jamii yetu kwa ujumla. Kwa sababu ya kuhangaikia zaidi kutoa “uthibitisho” wa Ukristo na utetezi wa “ushahidi unaodai uamuzi,” wafafanuzi na wahubiri wengi wa Kikristo wameacha kuisimulia Hadithi Kuu kama msingi wa huduma na utume wa Kikristo. Katika jitihada za kufikia na kugusa mioyo na akili za wale waliozoea mahubiri katika zama za kidijitali, wengi wameacha lugha ya asili ya Biblia kuhusiana na taswira, unabii, ushairi, na hadithi na kukumbatia zaidi mafundisho yanayohusu masuala ya “kisasa”, masuala ya maadili na mabadiliko ya kijamii kuliko kujishughulisha na aina za hadithi ambazo Hollywood kadhalika Biblia inasisitiza zaidi. Unadhani kwamba mkazo wa kisasa wa mafundisho kuhusu maadili ya kijamii na mihtasari ya moja kwa moja ya kitheolojia ni kusoma vibaya utamaduni? Je, unaamini nini—utamaduni unatafuta hadithi ambayo inaweza kuvuta usikivu na kuongoza mitazamo yake au maelezo ambayo yanaweza kutatua matatizo yake? Eleza. Je, Tunasoma Vibaya Alama za Utamaduni?
1
2
Hakuna Anayetimiza Ahadi Zake Siku Hizi
Wakati ambapo katika jamii kwa ujumla imekuwa nadra watu kuchukulia ahadi zao kwa uzito, tufanye nini ili hadithi ya ahadi ya Mungu iweze kuwa wazi na ya kuaminika? Katika jamii yetu ya leo, ahadi zinatolewa na kuvunjwa kwa urahisi wa ajabu sana: ahadi za ndoa zinaishia kuwa talaka za kutisha zenye kusababisha matengano, wanasiasa wanakula kiapo cha kulinda majimbo yao kisha baadaye wanashikwa katika ufisadi na unyanyasaji, wahubiri wanalia machozi ya mamba huku wakikiri majuto yao kwa sababu ya (kushikwa?) aibu na kashfa zao ambazo
3
Made with FlippingBook Annual report maker