https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

/ 2 3

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

Baada ya kukiri na/au kuimba Kanuni ya Imani ya Nikea (iliyopo kwenye viambatisho), omba maombi yafuatayo: Utupe neema, ee Bwana, kuitikia kwa utayari wito wa Mwokozi wetu Yesu Kristo na kuwatangazia watu wote Habari Njema za wokovu wake, ili sisi na ulimwengu wote tupate kuuona utukufu wa kazi zake za ajabu; anayeishi na kutawala pamoja nawe na Roho Mtakatifu, Mungu mmoja, milele na milele. Amina. ~ Episcopal Church. Kitabu cha Maombi ya Pamoja na Utoaji wa Sakramenti na Ibada Nyingine na Sherehe

Kanuni ya Imani ya Nikea na Maombi

za Kanisa, Pamoja na Zaburi au Zaburi za Daudi. New York: The Church Hymnal Corporation, 1979. uk 215

1

Hakuna jaribio katika somo hili.

Jaribio

Hakuna Maandiko ya kukariri katika somo hili.

Mapitio ya Kukariri Maandiko

Hakuna kazi za kukabidhi katika somo hili.

Kazi za Kukabidhi

MIFANO YA REJEA

Mungu wa Historia na Tamthilia ya Mungu

Katika ulimwengu ambao unaona imani ya Kikristo kama chaguo la utashi binafsi (sio kama imani iliyojengwa juu ukweli wa kihistoria), Wakristo wengi wameacha kuitetea imani yao ya Kikristo kama imani ya kihistoria. Sehemu kubwa za mrengo wa kiliberali wa madhehebu makuu zote zimeikana “historia” muhimu ya madai ya Kikristo kuhusu Yesu. Kwa mfano, kundi la Semina ya Yesu ( the Jesus Seminar , yaani, ile kamati maarufu sana ya utafiti wa kisomi iliyopewa kazi ya kutambua ni maneno gani katika Injili zetu yanayosemekana kwamba ni maneno ya Yesu, ambayo kwa kweli aliyasema Yesu mwenyewe), kamati hii ilidai kuwa iliweza kupata maneno machache tu yaliyotawanyika huku na kule, ambayo kamati ilikuwa tayari kusema kwa hakika labda ni habari sahihi za kihistoria kuhusu Kristo. Seminari nyingi zimechagua “utafiti wa kisayansi wa dini” ambao hauangazii kile ambacho Wakristo wameshikilia na kuamini katika karne zote, bali unaangazia kile ambacho sayansi inaweza kuthibitisha sasa kwa msingi wa uwezo wake wa kuthibitisha madai ya Ukristo. Mashambulizi haya na mengine yamefanya iwe vigumu kwa wengi kuukubali Ukristo kama hoja ya kihistoria isiyo

1

Made with FlippingBook Annual report maker