https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

2 2 /

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

nadharia. Ukweli huu umefichwa na jinsi wahubiri na wanatheolojia wanavyovutiwa kirahisi zaidi na nyaraka. Msomi mmoja wa Biblia amesema kwa usahihi kwamba Biblia inazungumza sana katika lugha ya picha. . . Hadithi, mifano, mahubiri ya manabii, tafakari za watu wenye hekima, taswira za wakati ujao, tafsiri za matukio yaliyopita, yote haya yanaelekea kuonyeshwa katika taswira zinazotokana na uzoefu. Mara nyingi hazitokei kwa lugha dhahania ya kiufundi. ~ Leland Ryken. Dictionary of Biblical Imagery . (toleo la kielektroniki). Downers Grove, IL: InterVarsity Press, 2000. Katika hadithi ya Injili picha za hadithi ya Mungu zinaonekana wazi wazi: Mwana Kondoo wa Mungu amewekwa juu ya mti kama dhabihu mbadala kwa ajili ya dhambi za ulimwengu. Kila mtu anayeamini kwamba huyu aliyekufa ni Kristo, kwamba alikufa na siku ya tatu akafufuka, atakombolewa kutoka katika dhambi zake, na kusamehewa adhabu yote mbele za Mungu, na kupewa Roho Mtakatifu ambaye atakaa ndani yake katika maisha haya yote, na kumfufua siku ya mwisho. Hadithi hii imerudiwa katika maisha ya mamilioni ya wanaume na wanawake, wavulana na wasichana, kwa zaidi ya miaka 2,000 ambao wanashikilia hadithi ya Yesu kama Habari Njema ya wokovu na uzima kwa watu wote. Umisheni unasimulia hadithi hii kwa watu wa ulimwengu, kwa lugha zao wenyewe, kwa njia ambazo wanaweza kuelewa na kuthamini upendo na neema ya Yule ambaye ni mwigizaji na mhusika mkuu wa hadhithi yake. Mungu ndiye Shujaa wa hadithi yake mwenyewe, na historia ya wokovu si kitu kingine chochote isipokuwa “Hadithi Yake”. Kwa imani, Hadithi ya utukufu wa Mungu inaweza kweli kuwa hadithi yetu wenyewe pale tunapoikumbatia. Ugunduzi upya wa kiini cha ujumbe wa Kikristo kama hadithi ni hitaji la lazima la wakati wetu, na ishara za theolojia mpya za “theolojia ya hadithi” na “theolojia simulizi” zinahitaji kurudi ili tupate kuelewa msingi wa uanafunzi na utume wa Kikristo. Msingi wa imani yetu ni hadithi kuhusu mhubiri mashuhuri Myahudi aliyedai kwamba Mungu ni Baba yake. Wale miongoni mwetu tunaoamini kwa hakika kwamba Yesu wa Nazareti alikuwa Masihi na Bwana wa wote tunashikilia hadithi hii kama tegemeo la maisha yetu, tumaini letu, na huduma yetu. Hebu tusisahau kamwe kwamba “Hapo zamani za kale” yetu hakika ina mwisho usemao: “Na wakaishi kwa furaha milele.” Kushiriki katika utume wa ndani na wa ulimwengu ni kutangaza hadithi hii, hadithi ya utukufu wa Mungu, kuishi kila siku papa hapa na sasa hivi mbele za Bwana anayeiandika kupitia sisi, mbele ya wale ambao bado hawajaisikia na kuielewa. Katika ulimwengu wa utume wa ulimwengu, kila wakati ni wakati wa hadithi.

1

Made with FlippingBook Annual report maker