https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

/ 2 1

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

Hivyo basi, haipaswi kuwa ajabu kwamba tunafafanua asili ya utume wa Kikristo kama kusimulia hadithi ya Yesu kwa wale wanaohitaji kuisikia. Umisheni daima umekuwa suala la kuchukua hatua ya kwenda kwa wale ambao hawajasikia Neno la upendo mkuu wa Mungu katika Yesu wa Nazareti na kuwasimulia hadithi hii kwa njia ambayo ni rahisi, ya wazi na yenye nguvu na ushawishi kwao. Kwa kuzingatia lugha yao, utamaduni wao, na kawaida zao za mawasiliano, tunatafuta kuifanya Injili ya neema ya Mungu iwe wazi katika muktadha wa utamaduni wao na jamii yao. Umisheni daima umekuwa kazi ya kusimulia hadithi ya utukufu wa Mungu katika Kristo tena na tena na tena. Lengo ni kwamba tuipeleke hadhithi hii mpaka miisho ya dunia ili kila watu wasikie, na wale wanaotubu na kuamini kweli ya hadithi hii wapate uzima wa milele. Kwa maneno ya moja kwa moja na ya wazi, hili linawakilisha mojawapo ya misingi mikuu ya utume wa Kikristo: kusimulia hadithi ile ya zamani ya Yesu na upendo wake. Kwa bahati mbaya katika duru kadhaa za Kikristo leo, wengi wameutupilia mbali ulimwengu wa Biblia ulioongozwa na hadithi, Injili ya Yesu, na mbinu ya utume inayotegemezwa na hadithi, huku wakikumbatia njia zenye mwelekeo wa kisayansi zaidi. Wakristo wengi wameacha nguvu ya hadithi na kufuata mbinu za kimantiki zaidi. Kwa hakika, katika baadhi ya makanisa yetu tumepoteza asili ya ajabu na yenye mguso inayotokana na usimulizi wa hadithi. Hadithi inaweka wazi ubora wa ukweli kwa njia ambayo maandishi ya kifalsafa au insha ya kisayansi haiwezi kamwe. Kwa kuweka msisitizo wao juu ya mahubiri ya ufafanuzi kwa kufuata mbinu za ufafanuzi zinazoaminika kisayansi ambazo zinakidhi vigezo vya ukosoaji wa kihistoria, waumini wengi wa Biblia wameiacha lugha yao ya asili na kukumbatia Injili kavu, ya kimantiki zaidi na isiyo na kina. Ingawa hawa wamechagua njia ya ulimwengu ili kuwasilisha ujumbe wa Injili, matokeo yamekuwa madogo na yasiyo na ushawishi. Kwa kukataa kusimulia hadithi, na kuisimulia vizuri, hatuushawishi ulimwengu wala hatuwi waaminifu kwa “lugha ya asili” ya Injili, ambayo ni kusimulia matukio ya kihistoria yahusuyo Kweli kwa njia ya hadithi ya Yesu wa Nazareti. Leland Ryken, kama wasomi wengine wachache wa kiinjili leo, anaangazia tabia ya Biblia ya kuzungumza kwa kutumia picha na hadithi badala ya lugha ya kiufundi. Anazungumza juu ya namna ambavyo tunakuwa wepesi kujiingiza katika makosa na kuteleza katika upepo wa kuona ujumbe wa Yesu kama muhtasari wa kitheolojia ulioambatanishwa na vielelezo: Kwa sababu ya Wakristo wengi kuichukulia Biblia kama kitabu tu kilichopo kwa makusudi ya kitheolojia na ibada, ni vigumu sana kutoingia kwenye kosa la kuitazama Biblia kama muhtasari wa kitheolojia wenye maandiko ya uthibitisho. Hata hivyo Biblia ni kitabu cha taswira na motifu (mada) zaidi kuliko kitabu cha dhahania na

1

Made with FlippingBook Annual report maker