Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

“viongozi vipofu” (Mt. 23:16) au “manabii wa uwongo” (Mt. 7:15). Kristo aliwakemea watu walipokuwa wamekosea, na aliwapongeza walipokuwa sahihi, lakini Yeye mwenyewe hakukaririwa kamwe kuwa alikubaliana na makosa yao—hakika si kwa kosa au upotofu wowote kuhusu Maandiko matakatifu. Bila shaka, wakosoaji wengine wanadai kwamba halikuwa suala la “kukubaliana,” bali ni suala la ukomo wa upeo linalofanya isiwezekane kutumia mamlaka ya Kristo kwa mambo ya kihistoria na nyeti ya Agano la Kale. Wakati fulani inaaminika, kwa mfano, kwamba ujuzi wa Yesu wa mambo haya “yasiyo ya kiroho” ulikuwa mdogo kwa sababu Yeye hakuwa Mungu kweli kweli. Hata hivyo, Yesu alitamka waziwazi kwamba Yeye ni Mungu, akitangaza kwamba Yeye ndiye “MIMI NIKO” wa Agano la Kale (Kut. 3:14) na Mwana wa Mungu Mwenyewe (Mt. 16:16-18; Mk 14:61 62). Madai haya ya uungu, Wayahudi wa zama zake waliokuwa na itikadi kali katika imani yao kwa Mungu mmoja, hawakupata shida kuyatafsiri. Walielewa moja kwa moja alichomaanisha. Yesu aliposema, “Mimi na Baba tu umoja” (Yh 10:30) wakaokota mawe ili wamwue, kwa sababu, walisema, “wewe uliye mwanadamu wajifanya mwenyewe u Mungu” ( mst . 33). Vivyo hivyo, Yesu alipomwambia yule mwenye kupooza, “Mwanangu, umesamehewa dhambi zako” (Mk 2:5), waandishi waliuliza swali sahihi kabisa, “Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu?” ( mst . 7). Na Yesu aliposema, “Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko” (Yh 8:58), hakuna ambaye hakuelewa dai lake la uungu (rej. “MIMI NIKO” wa Kutoka 3:14), maana kwa mara nyingine tena waliokota mawe ili wamwue. Kwa ushahidi zaidi kwamba Maandiko kwa ujumla yanafundisha uungu wa Kristo (taz. pia Mt. 26:64 85; Ebr. 1:8). Wengine wamesisitiza kwamba ujuzi wa Kristo uliwekewa mipaka kwa lile tendo lake la kuvaa mwili kama inavyoonyeshwa na ukweli

30

Made with FlippingBook Digital Publishing Software