Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

ya huduma ya Kristo. Kwanza, kwa habari ya mafundisho ya Yesu kuhusu uvuvio wa Agano la Kale, inapaswa kuzingatiwa kwamba mtazamo wowote kama huo wa “kukubaliana” unapingana moja kwa moja na moja ya mada kuu za huduma ya Kristo. Kwa sababu, hili si suala la hapa na pale, au kwamba Yesu alifanya marejeo machache ya Agano la Kale, bali ulikuwa msisitizo wa mara kwa mara na mkuu wa huduma yake. Ikiwa rekodi ya Injili hata inatoa kiini cha kile ambacho Yesu alisema (na kuna ushahidi wa kutosha kwamba inatoa zaidi ya hilo), 4 basi tunajua kwamba Yesu aliamini na kufundisha mamlaka ya kimungu ya Maandiko ya Agano la Kale. Zaidi ya hayo, kuhusu suala la Yesu kulithibitishwa Agano la Kale kama Kanoni, hakuna shaka kwamba Yesu hakukubaliana ilimradi na chochote kilichoaminiwa na Wayahudi . Yesu hakuwahi kusita kukemea maoni ya kidini yaliyokuwepo ambayo hayakuwa ya kweli, kama alivyofanya kwa Wayahudi ambao waliinua “mapokeo” yao juu ya “amri za Mungu” (Mt. 15:1-3). Mara sita katika Hotuba ya Mlimani aliweka kwenye mizani uthibitisho wake na tafsiri za uwongo za Kiyahudi za Agano la Kale, kwa maneno kama vile “Mmesikia kwamba imenenwa... lakini mimi nawaambia” (Mt 5:21-22, 27-28, 31-32, 33-34, 38-39, 43-44). Mara nyingi Yesu aliwaambia, kama katika Mathayo 22:29, “Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.” Alimkemea kiongozi mkubwa wa kidini Nikodemo, akisema, “Je! Wewe u mwalimu wa Israeli, na mambo haya huyafahamu [kuhusu kuzaliwa mara ya pili]?” (Yh 3:10). Yesu pia aliwaambia watu walipokuwa sahihi juu ya Agano la Kale, kama pale alipowaambia Mafarisayo kuhusu zaka, “hayo imewapasa kuyafanya” (Mt. 23:23), au kwa habari ya jibu la mwanasheria kuhusu upendo kuwa amri iliyo kuu zaidi, “Umejibu vema” (Lk 10:28). Kwa upande mwingine, walipokosea tu—ama kimaadili ama kikanuni—Yesu hakusita kuwaita

4 Ona Norman L. Geisler, “New Testament, Historicity of ” katika The Big Book of Christian Apologetics (Baker, 2012).

29

Made with FlippingBook Digital Publishing Software