Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

ya mwandishi na kitabu chake, kama pale aliposema, “Maana, Daudi mwenyewe asema katika chuo cha Zaburi” (Lk 20:42), au “aliyeandikiwa na Musa katika torati…” (Yh 1:45), au “Daudi katika Roho kumwita Bwana” (Mt. 22:43, taz. mst.42). Katika vifungu hivi na vingine, Yesu alionekana kwenda mbali zaidi ya jina la kitabu na kutoa jina la mwandishi wake. Swali muhimu la kujiuliza kuhusu kila kifungu ni: Ni nini ambacho Yesu anathibitisha? Ikiwa inaweza kuthibitishwa kwamba Yesu anathibitisha wazi wazi au anaashiria moja kwa moja ni nani mwandishi wa kitabu fulani, basi hii hakika itachukuliwa kama uthibitisho wa ukweli huo. Lakini bila kujali jibu la swali hili litakuwaje, hakuna shaka kwamba uthibitisho mwingi na wa kina wa Kristo kuhusu mamlaka, historia na uhalisi wa kanoni ya Kiyahudi ya Maandiko unadhihirisha wazi kwamba alikuwa akifundisha kweli hizi. Uthibitisho au Kukubaliana? Wakosoaji wengine wanadai kwamba Kristo hakuwahi kuthibitisha uvuvio, uhalali au uhalisi wa Agano la Kale hata kidogo. Wanadai kwamba Kristo hakujali kuhusu mambo haya ya urasmi na ya kiufundi hata kidogo, badala yake alichokifanya ni “kukubaliana” na mapokeo ya Kiyahudi yaliyokubaliwa siku hizo. Yaani, Yeye hakuwa akithibitisha, kwa mfano, ukweli wa kihistoria kwamba Yona aliwahi kukaa ndani ya nyangumi, bali alisema, akimaanisha kwamba, “Kama mnavyoamini kwamba Yona alikaa ndani ya nyangumi, kwa hiyo nataka kutumia mapokeo au hekaya hiyo iliyokubalika kukuonyesheni kwamba....” Kulingana na maoni haya, Yesu hakuwa anatoa uthibitisho kuhusu historia, uhalisi, sifa za kikanoni au mamlaka ya Agano la Kale, bali alikuwa akionyesha kukubaliana na masuala haya kama yalivyosadikika nyakati hizo. Janga la nadharia hii “ya kupendeza” ni kwamba inauawa na ushahidi wa kibabe na wa kweli, yaani mambo yanayotokana na sifa na maudhui

28

Made with FlippingBook Digital Publishing Software