Kristo: Mada Kuu Ya Biblia
6. Kuponywa kwa Naamani mwenye ukoma (Lk 4:26); 7. Miujiza ya Eliya kwa mjane (Lk 4:25); 8. Kuhifadhiwa kwa Yona ndani ya nyangumi (Mt. 12:41); 9. Unabii wa Danieli (Mt.24:15); 10. Unabii wa Isaya (Yh 12:38-41). Yesu aliyathibitisha haya, kama ambavyo pia alithibitisha kuhusu uwepo wa nafsi ya ibilisi (rej. Mt. 4:1-11), mapepo wasio na idadi (rej. Mk 5:1-13), mazungumzo yake yasiyo ya kawaida pamoja na Musa na Eliya, na miujiza mingi ambayo Yesu aliifanya katika siku zake mwenyewe. Hoja ya Kristo iko wazi: Agano la Kale ni maelezo ya kihistoria ya utendaji usio wa kawaida wa Mungu na watu wake. Baadhi ya wakosoaji wanadai kwamba marejeo ya Yesu kwa watu wa Agano la Kale kama Musa, Daudi, na Isaya hayapaswi kuchukuliwa kuwa uthibitisho wa mhusika kama mwandishi wa kifungu hicho bali kama tendo la kutambua tu uwepo wa kifungu husika. Hata hivyo, nyakati fulani Yesu anamrejelea mwandishi wa kitabu hicho. Kwa mfano, Yesu alirejelea sehemu zote mbili za Isaya (53:1 na 6:10) kama zinazotokana na mtu yule yule Isaya (Yh 12:38, 40), na vile vitabu vitano vya kwanza vya Agano la Kale kama “kitabu cha Musa” (Mk 12:26), “Torati ya Musa” (Lk 24:44), na wakati mwingine kama “Musa” (Lk 16:29; 24:27). Pia alizungumza kuhusu zaburi kama ya Daudi, lakini swali ni kama alitumia majina haya kwa ajili ya kudokeza eneo kinapopatikana kifungu kilichotajwa au kuthibitisha mtu aliyekiandika (au yote mawili). Kuna nyakati Yesu anarejelea kwa uwazi kitabu husika na wala si mtu aliyekiandika. Kwa mfano alipozungumza kuhusu “ kitabu cha Musa” (Mk 12:26), au “yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa” (Lk 24:44), au, “Isaya alitabiri vema.... kama ilivyoandikwa” (Mk 7:6). Hata hivyo, kuna nyakati ambapo Yesu anatofautisha kati
27
Made with FlippingBook Digital Publishing Software