Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

kilichowaka moto (Lk 20:37); (7) kutangatanga jangwani kwa Israeli (Yh 3:14); (8) hadithi ya Eliya na mjane (Lk 4:25); (9) na ile ya Naamani mwenye ukoma wa Shamu (Lk 4:27); (10) Daudi na hema ya kukutania (Mt. 12:3-4); (11) Sulemani na malkia wa Sheba (Mt. 12:42); (12) Yona na mji wa Ninawi (Mt. 12:41); (13) nabii Danieli (Mt. 24:15); (14) nabii Isaya (Yh 12:38-41). Ni dhahiri kwamba Yesu alithibitisha uhalisi wa kihistoria wa watu hawa na matukio haya kutokana na namna ya moja kwa moja ambayo anawarejelea na mamlaka ya mafundisho ambayo anayajenga kwa kutumia kielelezo cha watu na matukio husika. Kwa mfano, Yesu pale anaposema, “Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi” (Mt. 12:40), kimsingi anathibitisha kuwa matukio yote mawili ni ya kweli kihistoria. Yesu hangetafuta kufafanua ukweli kuhusu kifo na ufufuo wake kwa kutumia hadithi za kubuni kuhusu Yona. Uthibitisho wa Kristo wa Sifa ya Kimuujiza ya Matukio ya Agano la Kale Matukio ya Agano la Kale hayakuzingatiwa tu kuwa ya kihistoria lakini mengi ya matukio hayo yalikuwa ya tabia isiyo ya kawaida. Kwa msingi huo, marejeo ya Yesu yanathibitisha asili ya kimuujiza ya: 1. Uharibifu wa ulimwengu kwa gharika (Lk 17:27); 2. Mke wa Lutu kugeuka nguzo ya chumvi (Lk 17:32); 3. Kijiti kilichowaka moto mbele ya Musa (Lk 20:37); 4. Uponyaji wa Israeli kutokana na kuumwa na nyoka (Yh 3:14); 5. Mana kutoka mbinguni (Yh 6:49);

26

Made with FlippingBook Digital Publishing Software