Kristo: Mada Kuu Ya Biblia
Katika asili yake ya kibinadamu Yesu alikua katika maarifa kama mtoto (Lk 2:52). Lakini ukweli kwamba hakujua kila kitu kama mwanadamu haukanushi wala kubatilisha mamlaka ya kimungu ya kile alichojua na kufundisha. Na kama tulivyoona, alijua na kufundisha kwamba Yeye alikuwa Mwana wa Mungu na Biblia ni Neno la Mungu. Bila shaka, katika yale ambayo Yesu alifundisha alikuwa chini ya Baba. Yesu alitambua jambo hilo aliposema, “Baba ni mkuu kuliko mimi” (Yh 14:28) na “sikushuka kutoka mbinguni ili niyafanye mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenipeleka” (Yh 6:38). Mtume Paulo alifundisha vivyo hivyo alipoandika, “Kichwa cha Kristo ni Mungu” (1Kor. 11:3) na “Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote” (1Kor. 15:28). Hata hivyo, kuwekwa chini kwa Mwana kwa msingi wa ofisi na utendaji wake hakulazimu wala kumaanisha kuwepo kwa ukomo au mipaka katika ujuzi na asili yake. Mwana yuko chini kwa maana ya ofisi , lakini kwa asili Yeye ni sawa na Baba (Yh 10:30; 5:23; 1:1). Kuwekwa chini kwa Mwana kunatoa funzo tu kwamba kuna utaratibu katika Uungu, si kwamba kuna mipaka yoyote au makosa katika mafundisho ya Kristo. Maana, ni jambo moja kudai kwamba kulikuwa na mapungufu fulani ya kibinadamu katika ujuzi wa kibinadamu wa Yesu na ni jambo jingine kabisa kusema kwamba alikosea katika yale aliyoyafundisha. Kama ambavyo kuvaa mwili kulivyoweka mipaka fulani juu ya uungu wa Kristo usio na kikomo, na hata hivyo hakutenda dhambi kamwe (Ebr. 4:15; 1 Yh 3:5), vivyo hivyo mapungufu yoyote yanayoweza kuhusishwa na ufahamu wake, lazima ithibitishwe kwamba Yeye kamwe hakukosea katika jambo lolote alilofundisha (taz. Yh 8:40, 46). Kwa ufupi, hakuna ushahidi wa kizuizi chochote wala ukomo wowote juu ya ukweli wa yale ambayo Kristo alifundisha, na kwa hakika hakuna makosa katika mafundisho yake.
32
Made with FlippingBook Digital Publishing Software