Kristo: Mada Kuu Ya Biblia
DIBAJ I KITABU HIKI NI MATOKEO YA imani ya dhati kwamba Kristo ndiye ufunguo wa ufasiri wa Biblia, si tu kwa sababu Yeye ni utimilifu wa vivuli na unabii wa Agano la Kale, lakini kwa kuwa Kristo ndiye mada inayounganisha kipindi kizima cha ufunuo wa Maandiko. Kristo alisema mara kadhaa kuwa Yeye ndiye ujumbe mkuu wa Maandiko yote ya Agano la Kale (Lk 24:27, 44; Yh 5:39; Ebr. 10:7; Mt. 5:17). Kitabu hiki ni jaribio la kuchukulia kwa uzito uthibitisho wa Kristo aliposema, “Ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi” (Lk 24:44). Kama tutakavyoona katika kurasa hizi, namna hii ya kuiendea Biblia kwa kumtazama Kristo kama mada yake kuu, haikujikita zaidi katika utafiti wa vivuli, au hata katika unabii wa Agano la Kale, bali ni jaribio la kumwona Kristo kama kiunganishi cha ujumbe unaofunuliwa wa Maandiko Matakatifu kwa ujumla wake. Kristo anawasilishwa kama kiungo kati ya A.K na A.J, maudhui ya kanoni nzima ya Biblia, na mada unganishi ndani ya kila kitabu cha Biblia. Msisitizo uliopo hapa ni juu ya Kristo kama kiini cha umoja wa Biblia kwa kuzingatia sehemu kuu za Maandiko na mgawanyo wake. Kwa namna fulani, huu ni uchunguzi wa Biblia kwa muhtasari katika msingi wa ufunuo wa Kristo. Hakuna madhumuni ya moja kwa moja ya kitheolojia ya kitabu hiki, lakini kinashughulikia maswali ya kitheolojia, kama vile uvuvio wa Biblia na uungu wa Kristo. Hata hivyo, haya yanaibuka kutokana au kwa kuhusiana na mada kuu, ambayo ni kumtambulisha Kristo kama kiini cha ufasiri sahihi wa Biblia. Zaidi ya msukumo mkuu wa kitabu hiki, ambao ni kupendekeza baadhi ya njia za kuyaendea Maandiko kwa kuzingatia ufunuo wa Kristo,
7
Made with FlippingBook Digital Publishing Software