Misingi ya Utume wa Kikristo, Mwongozo wa Mkufunzi
2 0 0 /
MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO
kuhubiri habari njema kwa maskini. Alithibitisha umasihi wake kwa Yohana Mbatizaji kupitia matendo ya haki na kuwahubiria maskini. Alihakiki na kuthibitisha wokovu wa watu kwa kwa kuzingatia namna walivyowatendea maskini, na alijihusisha kikamilifu na “walio wadogo” (yaani, wenye njaa, wenye kiu, wageni, walio uchi, wagonjwa, na wafungwa). Kanisa ni jamii ya ufalme wa Mungu. Limeitwa kutangaza Habari Njema ya Ufalme kwa maskini, kutendeana kama mwili wa Kristo kila mmoja kwa mwingine, na kutoa ushahidi wa maisha ya Enzi Ijayo kwa kuonyesha kielelezo cha utendaji wa haki katika ulimwengu. Kupitia maisha na utume wa Kanisa, kwa uweza wa Roho Mtakatifu, Watu wa Mungu leo wanaonyesha na kufurahia shalom ile ile inayozungumzwa katika Agano la Kale. Kama mwili wa Kristo ulimwenguni, Kanisa limeitwa kuwa mtetezi wa maskini, ambayo ni alama ya utume halisi wa Kikristo. Kuhusu utume wa mijini, Kanisa limeitwa kutangaza Habari Njema kwa maskini, hilo ni pamoja na kuwaheshimu kama walivyochaguliwa na Mungu na kama watu ambao Kristo alijitambulisha nao. Hatupaswi kamwe kuwadhalilisha, bali kushughulika nao kwa haki na huruma, tukiwa na uhakika kwamba wanaweza kugeuzwa na kuchangia katika maendeleo ya Ufalme. Hatutakiwi kukidhi mahitaji yao kijuujuu tu, bali kujitahidi kushughulika na mifumo na mahusiano kwa namna ambayo itachochea hali ya haki zaidi, yaani kuishi “Injili ya mafanikio” ya kweli, ambayo ni kutafuta haki na usawa kwa niaba ya walio hatarini zaidi miongoni mwetu. Lengo letu la sehemu hii, Kanuni na Madokezo ya Kimisheni kwa ajili ya Kufanya Huduma Mjini , ni kukuwezesha kuona kwamba: • Yesu ndiye mwanzilishi na Kichwa cha Kanisa, Jamii ya Ufalme wa Mungu ya Agano Jipya, ambayo imeitwa kuonyesha shalom ya Mungu katikati ya watu wa Mungu leo. • Yesu alijitambulisha kama Masihi yule wa unabii na ahadi ya A.K. Alianzisha huduma yake ya Kimasihi kwa matendo ya kuponya walioonewa na kuhubiri habari njema kwa maskini. Alithibitisha umasihi wake kwa Yohana Mbatizaji kupitia matendo ya haki na kuwahubiria maskini. Alihakiki na kuthibitisha wokovu wa watu kwa kwa kuzingatia namna walivyowatendea maskini, na alijihusisha kikamilifu na “walio wadogo” (yaani, wenye njaa, wenye kiu, wageni, walio uchi, wagonjwa, na wafungwa). • Kanisa ni jamii ya ufalme wa Mungu. Limeitwa kutangaza Habari Njema ya Ufalme kwa maskini, kutendeana kama mwili wa Kristo kila mmoja kwa mwingine, na kutoa ushahidi wa maisha ya Enzi Ijayo kwa kuonyesha
4
Made with FlippingBook - Online catalogs