Misingi ya Utume wa Kikristo, Mwongozo wa Mkufunzi
/ 2 2 5
MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO
ni Mfalme wa shalom, pamoja na shalom kama kiwango cha maisha kwa watu wa Mungu. Umaskini ni kunyimwa shalom ya Mungu; baraka na upaji wake vilitolewa ili kuzuia kutokea kwa umaskini, na amri na maagizo ya Mungu kwa jamii ya agano zilikusudiwa kuhakikisha haki na uadilifu kati ya watu wa Yehova. Tukio la “Kutoka” lilijumuisha utambulisho wa Mungu pamoja na maskini na walioonewa, likifunua moyo wake wa haki na kuunda jamii yake ya agano ambayo iliitwa kuwa kielelezo cha utakatifu wake, taswira ya haki na rehema zake, na nuru kwa mataifa. Maandiko yamefafanua sababu kadhaa za umaskini, kutia ndani majanga ya asili na misiba (k.m., njaa, ukame, vimbunga, n.k.), uvivu na uzembe wa watu binafsi (k.m., maamuzi mabaya, tabia mbaya, uvivu, mioyo migumu, n.k.), na uonevu na matendo ya ukosefu wa haki yanayotendwa na watu wenye nguvu (k.m., unyanyasaji, unyonyaji, nk). Neno “maskini” katika Maandiko linahusianishwa na dhana mbalimbali zinazotumika kama visawe, kutia ndani “mjane,” “yatima,” na “mgeni.” Viwango au maagizo ya agano la Mungu yanaakisi moyo wake kwa ajili ya maskini na wahitaji, kutia ndani mambo kama vile maagizo ya Sheria (Torati) kuhusu mavuno na masazo yake, haki katika mahakama ambapo mambo yote, hatua zote, na shughuli zote zilipaswa kufanyika kwa uaminifu na kwa haki, bila kujali hali ya mtu; na rasilimali zilipaswa kugawanywa katika mwaka wa Sabato, na maskini walipewa sehemu ya mazao ya mashamba na mizabibu. Maana ya viwango hivi kwa jamii ya agano la Mungu iko wazi: katika shughuli zao zote, Watu wa Mungu walipaswa kuakisi moyo wa Mungu kwa maskini, kwa msingi wa ukombozi wa Mungu kwao wakati wa “Kutoka”, na walipaswa kuonyesha shalom ya Bwana katika mahusiano yao yote na kushughulika kwao na watu wengine. Yesu ndiye mwanzilishi na Kichwa cha Kanisa, Jamii ya Ufalme wa Mungu ya Agano Jipya, ambayo imeitwa kuonyesha shalom ya Mungu katikati ya watu wa Mungu leo. Yesu alijitambulisha kama Masihi yule wa unabii na ahadi ya A.K. Alianzisha huduma yake ya Kimasihi kwa matendo ya kuponya walioonewa na kuhubiri habari njema kwa maskini. Alithibitisha umasihi wake kwa Yohana Mbatizaji kupitia matendo ya haki na kuwahubiria maskini. Alihakiki na kuthibitisha wokovu wa watu kwa kwa kuzingatia namna walivyowatendea maskini, na alijihusisha kikamilifu na “walio wadogo” (yaani, wenye njaa, wenye kiu, wageni, walio uchi, wagonjwa, na wafungwa). Kanisa ni jamii ya ufalme wa Mungu. Limeitwa kutangaza Habari Njema ya Ufalme kwa maskini, kutendeana kama mwili wa Kristo kila mmoja kwa mwingine, na kutoa ushahidi wa maisha ya Enzi Ijayo kwa kuonyesha kielelezo cha utendaji wa haki katika ulimwengu. Kupitia maisha na utume wa Kanisa, kwa uweza wa Roho Mtakatifu, Watu wa Mungu leo wanaonyesha na kufurahia shalom ile ile inayozungumzwa katika Agano la Kale.
4
Made with FlippingBook - Online catalogs