Misingi ya Utume wa Kikristo, Mwongozo wa Mkufunzi
4 4 2 /
MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO
wakati wa msingi, muhimu, wa faida katika kila kitu wanachofanya watoto wa kuasili wa Mungu. Kuwaza kunakuwa laana tu ikiwa kunafanyika katika ubatili. ~ C. Seerveld. “Imagination.” The New Dictionary of Theology . S. B. Ferguson, mh. (toleo la kielektroniki). Downers Grove, IL: InterVarsity Press, 2000. uk. 331. Hakika, njia pekee ya kufikia kiini cha umisheni ni kupitia mafumbo: Mungu ni Bwana-harusi anayewavuta kwake watu watakaokuwa bibi-arusi wake na watawala pamoja naye katika enzi isiyo na mwisho, na Mungu ni shujaa wa vita ambaye hatimaye atamshinda ibilisi, mauti, na athari za laana, ili kuanzisha utawala mpya wa haki na amani. Taswira ya bibi-arusi na bwana-arusi inaonekana kwa uwazi katika Agano la Kale na Agano Jipya. Katika Maandiko, uhusiano wa ndoa umetumiwa mara kwa mara kuelezea uhusiano wa Mungu na watu wake. Israeli inaonyeshwa kama mke asiye mwaminifu wa Yahweh Mungu katika kitabu cha Hosea, mke ambaye Mungu amedhamiria kumrudisha katika upendo na uaminifu kamili katika Ufalme ujao. Maono haya haya yanatumika kuelezea ukaribu na mapenzi ya kina kati ya Kristo na Kanisa katika Agano Jipya, isipokuwa hapa Bwana mwenyewe kupitia utendaji wake wa moja kwa moja na kupitia huduma ya mitume analitayarisha Kanisa kama bibi-arusi bikira anayemsubiri bwana-arusi wake wa mbinguni (2 Kor. 11:2). Yohana Mbatizaji ni “rafiki wa bwana-arusi,” sawa na kile tunachokiita “msimamizi wa ndoa” leo, ambaye alimtayarishia Bwana njia (taz. Yoh. 3:29). Yesu alitumia mfano huu wa ndoa katika mafundisho yake ya Ufalme (taz. Mt. 22:1-14; 25:1-13), na ulitumiwa pia katika mafundisho ya mitume na maono ya kinabii (2 Kor. 11:2; Efe. 5:22-24; Ufu. 21:2, 9; 22:17). Vivyo hivyo, Bwana kama shujaa wa kiungu ndiye anayekuja kuponda kichwa cha nyoka, kama ilivyotajwa katika protoevangelium ya Mwanzo 3:15. Kila kipengele cha maisha na huduma ya Kristo kinaweza kutazamwa katika muktadha wa yeye kuwa Mwana wa Adamu wa kiungu aliyekabidhiwa jukumu la kuwashinda maadui wa Mungu na kuleta utawala wa Mungu kwa furaha na nguvu. Kwa mfano, Leland Ryken anatoa muhtasari wa Kristolojia ya Paulo kwa kutumia taswira ya shujaa wa kiungu kama msingi wa kuielewa elimu ya Kristo: Hivyo basi, Paulo aliweza kutazama nyuma katika kifo, ufufuo na kupaa kwa Yesu Kristo kwa kutumia taswira ya shujaa wa kiungu. Kwa mfano, katika Wakolosai 2:13 15, anamalizia hoja yake kwa lugha ya shujaa wa kiungu: “akiisha kuzivua enzi na
Made with FlippingBook - Online catalogs