Mtaala wa Cornerstone, Kitabu cha Mwanafunzi

SOMO LA 2 | KUTAF S I R I B I B L I A : MB I NU YA HATUA TATU / 107

Lengo letu katika sehemu hii, Kuziba Pengo kati ya Ulimwengu wa Kale na wa Sasa , ni kukuwezesha kuona kwamba: • Mbinu ya Hatua Tatu ni mbinu fasaha ya kutafsiri Biblia iliyotengenezwa ili kutusaidia kuelewa kweli za maandiko na kuziba pengo kati ya ulimwengu wa kale na wa sasa. • Maana ya wazi na fupi ya Mbinu ya Hatua Tatu ni “kuelewa maana iliyokusudiwa katika mazingira ya kwanza ya andiko ili tuweze kugundua kanuni za jumla za Kweli ya Neno ambazo zinaweza kutumika katika maisha yetu binafsi ndani ya uhuru wa Roho Mtakatifu.” • Ingawa kusoma maneno mahususi, vifungu vya maneno, aya, sura, sehemu, na vitabu vya Biblia ni jambo la kujenga na la lazima, ufahamu wetu wote katika maandiko unapaswa kuendana na ujumbe wa Biblia nzima, yaani, maana na ujumbe wa ufunuo wa mwisho wa Mungu kwetu katika nafsi na kazi ya Yesu Kristo. • Mbinu ya Hatua Tatu inaakisi na kuendana na mbinu ya sarufi ya kihistoria ya kutafsiri maandiko, ambayo inahakiki na kuthibitisha maana ya wazi ya maandiko katika Biblia, ufunuo endelevu wa Mungu kwa njia ya Kristo, umoja wa Biblia, na usahihi wa andiko katika kuwasilisha ujumbe kwetu kwa kutumia tanzu na miundo tofauti ya fasihi. • Kila hatua inayohusika katika Mbinu ya Hatua Tatu ina lengo na mantiki yake mahususi, kadhalika ina sababu na msingi, na mitazamo muhimu, na inatimizwa kwa fuata mpangilio na orodha maalum ya vipengele. Ili kuweza kutumia mbinu hii, lazima tuwe na ufahamu na ujuzi kuhusiana na hatua husika na vipengele vyake. • Katika kujiandaa kutumia njia yoyote ya kujifunza Biblia, jambo kubwa na la msingi zaidi ni mtazamo wa mwanafunzi wa maandiko, kwa sababu hatua hizi za kujifunza kupitia Mbinu ya Hatua Tatu zinadai unyenyekevu, bidii, na uhuru katika kila hatua. • Kama watumwa wa haki chini ya ubwana wa Kristo, tumeitwa kulitii Neno lake katika kila nyanja ya maisha na huduma zetu, kwa hiyo, namna yoyote halali ya kutafsiri Biblia lazima ilenge katika kulifahamu Neno la Mungu kwa madhumuni ya kuleta badiliko katika maisha , na si habari ya kujaza taarifa akilini.

2

M A S O M O Y A B I B L I A

Made with FlippingBook Digital Proposal Maker