Mtaala wa Cornerstone, Kitabu cha Mwanafunzi

108 / MTAALA WA CORNERS TONE K I TABU CHA MWANAFUNZ I

Kila Mtu Ana Mfumo wa Kutafsiri Biblia Amini usiamini, kila mtu ana mbinu ya kutafsiri Biblia. Lakini sio mbinu zote zina faida sawa. Wengine hutumia mbinu ya ubashiri wa kidole. Hii inahusisha kufuata maelekezo fulani yanayodaiwa kuwa ya kiroho, kutafuta mstari fulani – kwa kawaida kwa kufumba macho – na kuchukua sehemu hiyo ya maandiko kama jibu au kweli iliyotolewa na Mungu. Tunaweza kucheka kusikia hilo, lakini mara nyingi tunapopuuza muktadha wa andiko, hatuna tofauti kabisa na mtu anayetumia mbinu ya kubahatisha andiko. Kisha kuna wale ambao wanasoma Biblia sana, lakini kamwe hawaonekani kupiga hatua kubwa sana katika kuielewa. Wanaweza kunukuu maandiko mengi tena kwa urefu sana, lakini wanapata shida kuelewa maana ya andiko. Wengine hufuata njia ya msukumo wa ndani. Wanasoma tu kile “kinachowasisimua”wakati huo, kana kwamba Biblia ilikusudiwa kuwafanya wajisikie vizuri daima. Watu hawa wote wana mifumo ya kutafsiri Biblia, na si vigumu kuona ni kwa nini mbinu hizo hazileti uzima wa kiroho. Kama matokeo ya mbinu hizi—ambazo kwa hakika kwa sehemu ni mbinu za kujifunza Biblia na kwa sehemu ni njia za kutafsiri Biblia—wengi wanaozitumia ni dhaifu kiroho na wamekatishwa tamaa ya kupata kitu chochote cha maana kutoka katika Biblia. Mazoea kama hayo hayaleti kamwe ukomavu katika kulitumia Neno la Mungu kwa namna yenye nguvu na iwezayo kuzaa matunda. Mbinu za kutafsiri zinaweza kuwa za kubahatisha au za kufuata mfumo mahususi, na hata kutafsiri kwa kufuata mfumo kunaweza kuleta manufaa, au kusiwe na faida na badala yake kukaharibu maana halisi ya Neno la Mungu. Shauku ya Mungu ni kwamba waamini wafike mahali ambapo wanaweza kusoma Biblia kwa namna yenye uelewa, uwiano na wepesi katika kuhusianisha andiko na andiko ili kupata ujumbe kamili wa Biblia.

2

M A S O M O Y A B I B L I A

~ Paul Karleen. The Handbook to Bible Study . (Toleo la Kielektroniki). New York: Oxford University Press, 1987.

I. Maana, dhumuni, vipengele, na faida za Mbinu ya Hatua Tatu ya kutafsiri Biblia

Muhtasari wa Maudhui ya Video

A. Maana: “kuelewa maana iliyokusudiwa katika mazingira ya kwanza ya andiko ili tuweze kugundua kanuni za jumla za Kweli ya Neno ambazo zinaweza kutumika katika maisha yetu binafsi ndani ya uhuru wa Roho Mtakatifu.”

Made with FlippingBook Digital Proposal Maker