Mtaala wa Cornerstone, Kitabu cha Mwanafunzi
SOMO LA 3 | USHAHIDI WA AGANO LA KALE KUHUSU KRISTO NA UFALME WAKE: KUTOLEWA KWA AHADI / 139
waliberali wamefikia hatua ya kulishutumu Agano la Kale kama zao la utamaduni wa zamani ambao mawazo yake ya kitheolojia na kimaadili yaliakisi enzi na mazingira yao zaidi kuliko mambo ambayo sisi kama “Wakristo wenye akili na wastahimilivu” tungeweza kuyaona kuwa yenye kukubalika. Je, tunapaswa kufanya nini kuhusu majaribio haya ya kisasa ya kutofautisha kati ya Mungu wa Agano la Kale na Mungu wa Agano Jipya, kama alivyofunuliwa kwa njia ya Yesu wa Nazareti? Je, kuna mwendelezo gani kati ya maagano hayo mawili? Je, tukubali, kwa namna yoyote, kwamba kunaweza kuwa na tofauti kati ya Mungu wa Agano la Kale na Mungu wa Agano Jipya? Elezea. Yesu na Maana ya Agano la Kale Yesu wa Nazareti aliporejelea Biblia au Maandiko, alirejelea Agano la Kale. Leo, AK linarejelewa katika duru zisizo za Kikristo kama “Biblia ya Kiebrania,” na kuna mijadala mingi kuhusu maana ya Agano la Kale. Kwa Wakristo wengi, mamlaka ya juu na bora zaidi kuhusiana na maana ya Agano la Kale ni Yesu, ambaye bila shaka katika angalau vifungu vitano tofauti katika Agano Jipya alisema kwamba yeye mwenyewe ndiye alikuwa mada ya Biblia ya Kiebrania (rej. Lk 24:25-27, 44-48; Mt. 5:17-18 ; Yoh. 5:39-40; 1:14- ling. Zab. 40:6-8). Maandiko haya yanaonyesha kwamba Yesu aliamini kwamba Agano la Kale, Biblia ya Kiebrania, kimsingi lilikuwa ni Maandiko ambayo yalielekeza wasomaji wake kwa Masihi, yaani Yeye mwenyewe, kwa maana ya vivuli na unabii, na kwamba usomaji sahihi wa Agano la Kale ulipaswa, kwa maana fulani ya msingi, kupata maana yake katika nafsi yake. Kauli hii, hata hivyo, ilikuwa kiini cha mgogoro wa mara kwa mara kati ya Yesu na walimu wa Biblia wa nyakati zake; madai kama hayo, kwamba Maandiko yote yalifikia utimilifu wake wa kitheolojia na wa kiroho katika Yeye kama Masihi wa Mungu, kwao yalichukuliwa kama yasiyokubalika, na hata kama kukufuru. Namna hii ya matumizi ya Biblia katika msingi wa Kristo kama kiini na ujumbe wake mkuu una utata leo vile vile, hasa katika ulimwengu wa ukosoaji wa Biblia, ambao unaona mtazamo kama huo wenye mwelekeo mmoja tu kwa Maandiko yenye aina mbalimbali za fasihi kuwa wenye matatizo. Unafikiri nini juu ya hili? Kulingana na kile unachojua leo, unawezaje kuelewa asili ya Agano la Kale katika uhusiano wake na Yesu Kristo? Je, ni kwa kiwango gani unaweza kusimamia aina hii ya hemenetiki pasipo kupotosha au kutafsiri vibaya ujumbe wa msingi wa Agano la Kale?
3
3
M A S O M O Y A B I B L I A
Made with FlippingBook Digital Proposal Maker