Mtaala wa Cornerstone, Kitabu cha Mwanafunzi
152 / MTAALA WA CORNERS TONE K I TABU CHA MWANAFUNZ I
MIFANOHALISI
Kabla Halijawa Agano la Kale Kwenu, Lilikuwa Biblia Yetu ya Kiebrania Vurugu za magenge zimekuwa zikiongezeka katika jamii yako kwa muda. Katika kuonyesha umoja na uungaji mkono, vikundi mbalimbali vya kidini vimetuma wawakilishi wao kwenye mjadala wa kiekumene kuhusu jeuri, uvumilivu, na heshima kwa wengine. Mmoja wa washiriki wa jopo alipoanza kutoa maoni yake kuhusu “Agano la Kale” rabi wa eneo hilo kwa uchangamfu lakini kwa mkazo mkubwa alitoa maelezo yafuatayo: “Kama nijuavyo kwamba wafuasi wengi wa Kristo, waamini Wakristo, wako katika hadhira hii, na kwamba ni kawaida yao kurejelea sehemu ya kwanza ya Biblia zao kama Agano la Kale; ningependekeza kwamba kwa wakati huu ambao tutakuwa pamoja hapa, tungerejelea Agano la Kale la Kikristo kama Biblia ya Kiebrania. Unajua, kwetu sisi, wanaoamini dini ya Kiyahudi, hiki hakijawahi kuwa kitabu cha zamani; ni Maandiko yetu na tunayarejelea kama Maandiko yetu ya Kiebrania. Je, litakuwa jambo gumu sana kwetu kukirejelea kwa njia hii, tunapozungumza pamoja kuhusu heshima, umoja, na kusaidiana sisi kwa sisi?” Je, ungemjibuje rabi katika muktadha huu? Je, kauli hii ya rabi ni kama dhamira ya kufanya mambo kuwa magumu bila sababu, au kuna jambo lolote muhimu kuhusu kukataa kuliona Agano la Kale kama sehemu ya zamani ya Biblia? Kuichukulia “Biblia ya Kiebrania” kama “Agano la Kale” kunapunguzaje uwezo wetu wa kuona umuhimu wake kwa Wakristo leo? Agano la Kale na Huduma ya KuwakamilishaWatakatifu Ni wazi kabisa kwamba Maandiko ambayo Paulo aliyataja katika 2 Timotheo 3, ambayo yangeweza kumfanya mwanamke au mwanamume mtumishi wa Mungu kufaa kwa ajili ya kazi ya huduma, yalikuwa Agano la Kale. Kimsingi, Biblia ya Yesu na mitume ilikuwa Agano letu la Kale, na kutokana na usomaji wa harakaharaka wa nyaraka tunaona kwamba walilinukuu na kulirejelea mara kwa mara katika uandishi wao kwa waumini wapya na makutaniko machanga. Hata hivyo, ni vigumu katika nyakati za sasa kupata vitini vya masomo ya ufuatiliaji na mitaala ya uanafunzi ambapo mafundisho, hadithi, vielelezo, na unabii wa Agano la Kale vinatumika kama msingi wa masomo hayo. Kwa namna fulani, Agano la Kale ni kama liko katika aina fulani ya uhamisho katika mazingira mengi ya kanisa la kiinjili. Linasomwa mara chache, na mara nyingi hata huhubiriwa kwa nadra. Hadithi fupi hapa, mithali kidogo pale, lakini ni mara chache sana ambapo tunaweza kuwapata hata wafafanuzi wa maandiko wakitumia majuma au miezi katika fasihi ya Agano la Kale ili kuwafundisha Wakristo. Ni wazi kwamba upuuziaji huu umezalisha aina fulani ya ujinga kuhusiana na Agano la Kale kwa Wakristo wengi, ambao hawajawahi kupata mafundisho
1 Ukurasa wa 88 8
3
M A S O M O Y A B I B L I A
2
Made with FlippingBook Digital Proposal Maker