Mtaala wa Cornerstone, Kitabu cha Mwanafunzi

SOMO LA 4 | MUNGU ROHO MTAKAT I FU : NAF S I YA ROHO MTAKAT I FU / 245

Mungu Roho Mtakatifu Nafsi ya Roho Mtakatifu

S OMO L A 4

Ukurasa wa 127  1

Karibu katika Jina lenye nguvu la Yesu Kristo! Baada ya kusoma, kujifunza, kushiriki katika mijadala, na kutendea kazi yaliyomo katika somo hili, utakuwa na uwezo wa: • Kutoa muhtasari wa mtazamo wa Agano la Kale kuhusu Roho wa Mungu. • Kutumia Maandiko kuelezea kazi ya Roho Mtakatifu ya kutoa uzima katika kuumba na kuuhifadhi ulimwengu. • Kutambua ishara kuu zinazohusiana na Roho Mtakatifu katika Maandiko na kuonyesha ni kwa namna gani zinachangia katika uelewa wetu juu ya Roho kama mpaji wa uzima. • Kuelezea ni kwa namna gani majina na vyeo vya Roho Mtakatifu vinatusaidia kumwelewa kama mpaji wa uzima. • Kuelezea kwanini huduma ya Roho ni chanzo cha tumaini. Roho Anayemfanya Mungu Ajulikane Soma 1 Wakorintho 2:10-11 na Warumi 8:26 . Roho wa Mungu ni wa ajabu sana. Kwa upande mmoja, anafunua mafumbo ya ndani kabisa ya nia na mapenzi ya Baba. Ana maarifa na ufahamu usio na kikomo. Na bado, kwa upande mwingine, anayo huduma maalum ya kuwa karibu nasi, ili kutusaidia kuelewa Mungu ni nani na ni kitu gani anatamani kwetu. Roho Mtakatifu, kwa mujibu wa mafundisho ya 1 Wakorintho 2, ndiye anayetufunulia hekima na siri za Mungu zilizofichika. Na, kama vile somo la Warumi linavyoonyesha, Roho huomba mapenzi ya Mungu ndani yetu na kupitia sisi wakati ambapo fahamu zetu za kibinadamu zimefikia kikomo na hatujui nini au jinsi gani tunapaswa kuomba. Tunapoanza somo letu la theolojia ya Roho Mtakatifu, tunakumbana na kweli kuu kwamba hatuwezi kumwelewa Roho wa Mungu pasipo msaada wa Roho wa Mungu. Ikiwa kwa kweli tutaufahamu ukweli huu, utaweza kuzalisha unyenyekevu na shukrani ndani yetu. Tunanyenyekezwa kwa sababu tunatambua kwamba hatuwezi kumjua Mungu kwa juhudi zetu wenyewe (haijalishi tunajifunza kwa bidii kiasi gani), bali kwa kazi ya Roho pekee. Tunashukuru kwa sababu tunajua kwamba tumempokea Roho kupitia ahadi za kweli za Mungu na kwamba tayari yuko kazini ndani yetu na kati yetu ili kutuongoza kwenye kweli yote.

Malengo ya Somo Ukurasa wa 127  2

Ibada Ukurasa wa 127  3

4

T H E O L O J I A N A M A A D I L I

Made with FlippingBook Digital Proposal Maker