Mtaala wa Cornerstone, Kitabu cha Mwanafunzi

36 / MTAALA WA CORNERS TONE K I TABU CHA MWANAFUNZ I

d. Yesu aliingia na kuishi katika ulimwengu kwa njia ya unyenyekevu, ya kawaida kuliko inavyoweza kuelezewa (2Kor. 8:9).

2. Atakaporudi, tutatoa hesabu kwa Bwana wetu kuhusu namna tulivyowatendea maskini wakati wa uhai wetu (Mt. 25:31-46).

a. Itabidi tutoe ushahidi wa kile tulichofanya ili kutengeneza njia za fursa kwa wale wanaoishi katika hali ya umaskini (Mt. 25:35-36, 42-43).

b. Yesu alilinganisha kuwatunza watu walio na njaa, wenye kiu, wageni, walio uchi, wagonjwa, na wafungwa gerezani kama kumtunza yeye (Mt 25:40, 45).

1

K A Z I Y A K I U K O M B O Z I D H I D I Y A U M A S K I N I

c. Hili halifanyiki ili kupata wokovu, bali ni kuishi tukizingatia neema tuliyopewa na Kristo (Efe 2:8-10).

C. Yesu alionya dhidi ya utajiri.

1. Yesu alifundisha kwa mkazo dhidi ya dhana iliyotawala kwamba kuwa tajiri ni ishara ya uhaka wa wokovu (Mt. 19:23-30).

2. Alifundisha kwamba pesa ndicho kitu cha kwanza tunachohitaji kujilinda nacho kisifanyike kuwa sanamu (Mt. 6:24).

3. Alifundisha kwamba fedha hazina wamiliki, ni watumiaji tu na kwamba hatupaswi kuweka utambulisho wetu katika mali (Luka 12:13-21).

Made with FlippingBook Digital Proposal Maker