Mtaala wa Cornerstone, Kitabu cha Mwanafunzi

458 / MTAALA WA CORNERS TONE K I TABU CHA MWANAFUNZ I

1. Mungu alimpenda kila mtu katika dunia nzima, aliye hai, aliyekufa, na ambaye bado hata hajazaliwa pasipo vigezo wala upendeleo.

a. 2 Kor. 5:19

b. 1 Yoh. 4:9-10

c. Lk. 12:7

2. Thamani ya upendo wa Mungu inaonyeshwa katika dhabihu ya Mwanawe wa pekee kwa ajili ya kila mmoja, Mt. 18:14.

3. Mungu hakumtuma Mwanawe ili ahukumu, bali kuwaokoa wote waliomo duniani.

4. Maana: Neema ya Mwenyezi Mungu isiyo na mwisho na isiyo na kikomo iko juu ya kila mwanadamu, ingawa pengine hawajui .

4

U T U M E K A T I K A M I J I

F. Mungu anajihusisha na mapambano, mahitaji, na mizigo ya wale walio wanyonge zaidi na wenye kuumizwa miongoni mwetu. Zab. 146:5-9 – Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, Na tumaini lake ni kwa Bwana, Mungu wake, 6 Aliyezifanya mbingu na nchi, Bahari na vitu vyote vilivyomo. Huishika kweli milele, 7 Huwafanyia hukumu walioonewa, Huwapa wenye njaa chakula; Bwana hufungua waliofungwa; 8 Bwana huwafumbua macho waliopofuka; Bwana huwainua walioinama; Bwana huwapenda wenye haki; 9 Bwana huwahifadhi wageni; Huwategemeza yatima na mjane; Bali njia ya wasio haki huipotosha.

1. Mungu ana mzigo kwa ajili ya wanadamu wanaoonewa, wenye njaa na wanaonyanyaswa kila mahali.

Made with FlippingBook Digital Proposal Maker