Mtaala wa Cornerstone, Kitabu cha Mwanafunzi
SOMO LA 1 | UONGOFU NA WI TO : NENO L I NALOUMBA / 95
• Je, kuna uhusiano gani hasa kati ya Neno la Mungu katika Yesu na Neno la Mungu katika Maandiko? Lipi linapaswa kupewa uzito zaidi ya lingine? Au je, yamekusudiwa kuchukuliwa na kuheshimiwa kwa kiwango sawa? • Je, tunapaswa kuhusianaje na Roho Mtakatifu, kivitendo, ili tuweze kujua kwa hakika kwamba atatufundisha tunapojifunza Neno la Mungu? • Ikiwa nitajifunza Neno la Mungu katika muktadha wa kusanyiko, kuna umuhimu gani wa kuwa na muda wangu binafsi wa kujifunza Neno la Mungu? Je, ikiwa sikubaliani na baadhi ya mambo ambayo yanafundishwa katika kanisa langu, au na mchungaji wangu – nifanyeje? Kesi Nzito ya Kutoelewana Wakati kanisa fulani limekuwa na mfululizo wa mafundisho juu ya Ujio wa Pili wa Kristo, binti mmoja ambaye ni kiongozi kijana wa Kikristo amekumbana na mafundisho katika mahubiri ya mchungaji ambayo hayaelewi, na, kwa mtazamo wa haraka haraka, hakubaliani nayo. Ametumia muda fulani kujadiliana na mchungaji baadhi ya mambo hayo ambayo kijana huyo anapingana nayo, na hakuna hata moja kati ya hayo ambalo ni la msingi sana, kwa maana ya kwamba linakinzana na jambo lolote linalofundishwa katika Maandiko. Mchungaji ameweka wazi kwamba haya ni maoni yake tu kuhusu Maandiko, lakini ni mwalimu mwenye nguvu na wengi wanaona mawazo yake kuwa yenye mantiki. Mchungaji ni kiongozi wa kibiblia, mwalimu mzuri wa Kikristo, na ndugu mnyenyekevu katika Kristo. Dada huyu anapaswa kufanya nini katika hali hii? kikundi cha vijana analazimika kuandika andiko la muhula kuhusu nadharia ya mageuzi. Mwanafunzi huyu huyu amekuwa akijifunza kanisani jinsi Mungu alivyoumba ulimwengu kupitia Neno lake, na kimahususi zaidi, kupitia Yesu Kristo. Anayaamini Maandiko, kwamba fundisho la Biblia kuhusu uumbaji ni sahihi, na bado Biblia haionekani kuzungumzia masuala yote anayokabiliana nayo darasani kuhusu sayansi. Hataki kugeuza darasa lake la sayansi kuwa kikundi cha mazungumzo ya kidini, lakini anatatizika kutafuta njia ya kuzungumzia maoni ya Biblia kuhusu uumbaji katika darasa lake la sayansi katika shule ya sekondari. Ikiwa ndugu huyo mchanga angekujia ili kupata ushauri, ungemshauri afanye nini au asifanye nini? Kukana Imani? Katika darasa la sayansi shuleni, mmoja wa wanafunzi katika
MIFANOHALISI
1
1
Ukurasa wa 72 9
M A S O M O Y A B I B L I A
2
Made with FlippingBook Digital Proposal Maker