The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide
/ 1 1 1
UFALME WA MUNGU
Bila shaka una maswali fulani juu ya somo la eskatolojia, na mafundisho ya Biblia juu ya kifo na hali ya wafu. Tafadhali chukua muda mwingi uwezavyo kujibu maswali haya na mengine ambayo yaliibuka kutokana na maudhui ya video. Jibu kwa uwazi na kwa ufupi, na inapowezekana, tumia Maandiko. 1. Nini maana ya istilahi ya kitheolojia “eskatolojia”? Kwa nini mahubiri na masomo ya eskatolojia yawe kipaumbele katika mitaala ya mtendakazi yeyote Mkristo, mchungaji, au mmishenari wa mjini? 2. Je, ni baadhi ya sababu zipi ambazo Maandiko yanatoa kwa Kanisa kwamba ni lazima tujifunze mafundisho ya mambo ya mwisho kwa kushirikiana na utimilifu wa Ufalme? 3. Je, Wakristo wanapaswa kuhuzunika kwa sababu ya kifo cha wapendwa wao kama wale wasiomjua Bwana? Kwa nini ndio au kwa nini hapana? 4. Kwa nini ni lazima kwa waamini wanaoshikamana na tumaini la Kukamilishwa kwa Ufalme kuwa na kiasi na kukesha kuhusu wakati wa kutokea kwa Kristo? 5. Eleza tofauti kati ya eskatolojia ya mtu binafsi na ya ulimwengu. 6. Je, ni baadhi ya mambo gani ya jumla yanayofundishwa katika Maandiko kuhusu kifo? Kuna tofauti gani kati ya kifo cha kimwili na kiroho? Je, vinanafananaje? 7. Ni zipi athari kuu za kifo zinazotajwa katika Maandiko? Ni zipi baadhi ya tofauti kati ya maana ya kifo kwa asiye Mkristo na maana ya kifo kwa Mkristo? 8. Ni nini maana ya neno la kitheolojia “hali ya wafu,” na kwa nini ni muhimu kuwa na ufahamu huu kwa ajili ya kuwahudumia waliofiwa? 9. Unaweza kufafanuaje maoni ya hali ya wafu kama “usingizi wa nafsi” na “toharani”? Je, kuna ushahidi gani wa kibiblia kwa maoni haya, na je, unayaona kuwa ya kushawishi? 10. Bainisha mtazamo wa hali ya wafu kuwa ni uwepo wa Bwana kwa Wakristo pekee. Je, unaona ushahidi wa kibiblia hapa kuwa wenye kushawishi? Kwa nini ndio au kwa nini hapana?
Sehemu ya 1
Maswali kwa Wanafunzi na Majibu
ukurasa 349 8
4
Made with FlippingBook Learn more on our blog