The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide

1 1 2 /

UFALME WA MUNGU

Kukamilishwa kwa Utawala wa Mungu Sehemu ya 2

Mch. Dkt. Don. L. Davis

Mambo ya jumla yanayohusiana na kukamilishwa kwa Ufalme wa Mungu ni Ujio wa Pili wa Yesu Kristo, ufufuo wa wafu na hukumu ya mwisho, na Mungu kuwa Yote-katika-yote. Malengo yetu ya sehemu hii ya pili ya Kukamilishwa kwa Utawala wa Mungu ni kukuwezesha: • Kubainisha vipengele muhimu vinavyohusiana na Ujio wa Pili wa Yesu Kristo ili kukamilisha Ufalme wa Mungu duniani. • Kueleza waziwazi mafundisho ya Maandiko yanayohusiana na ufufuo wa wafu na hukumu ya mwisho. • Kufahamu hali ya mwisho ya Ufalme uliokamilishwa, wakati Mungu Mwenyezi atakapokuwa Yote katika yote kwetu.

Muhtasari wa Sehemu ya 2

ukurasa 349  9

4

I. Ufalme Utakamilika Katika Ujio wa Pili wa Yesu Kristo.

Muhtasari wa Sehemu ya 2 ya Video

A. Ujio wa Yesu Kristo ( parousia ) hakika utatokea, na utakuwa wa uhakika.

1. Parousia , ambayo inaweza kutafsiriwa kama “kuwapo” au “kuja” mara nyingi huhusishwa na kurudi kwa Yesu, ambako alitaja mara nyingi katika mafundisho yake, kama vile katika Mathayo 24:30 na 26:64.

2. Petro anarejelea uhakika wa kuja kwa Yesu, Mdo. 3:19-21.

3. Paulo hana shaka na Roho wa Bwana kuthibitisha uhakika wa kuja kwa Kristo, 1 Thes. 4:15-16.

Made with FlippingBook Learn more on our blog