The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide

1 1 4 /

UFALME WA MUNGU

c. Yesu hatatuma wawakilishi, wabadala, au wajumbe mahali pake wakati wa kukamilisha Ufalme wa Mungu ufikapo. Atakuja mwenyewe, binafsi.

2. Kuja kwake kutakuwa katika mwili .

a. Kuja kwake kutakuwa katika mwili, halisi, si kiroho au kiakili, Mdo 1:11.

b. Ujio wa kibinafsi utakuwa katika mwili ule ule ambao alipaa nao mbinguni.

3. Kuja kwake kutaonekana .

a. Yesu anasema kuja kwake kutaonekana mawinguni, na kwamba mataifa yataomboleza yatakapomwona akija juu ya mawingu ya anga, pamoja na nguvu na utukufu mkuu, Mt. 24:30.

4

b. Kuja kwa Kristo kutaonekana kwa macho ya wale wote watakaokuwa hai duniani.

4. Kuja kwake kutajawa na fahari na utukufu .

a. Ujio huo unafafanuliwa katika Injili za Zinoptiki (Injili ndugu) kama Bwana wetu Yesu akija juu ya mawingu kwa nguvu nyingi na utukufu, Mt. 24:30; Marko 13:26; Luka 21:27.

b. Utatangazwa kwa mlio wa tarumbeta ya malaika mkuu, 1 Thes. 4:16.

Made with FlippingBook Learn more on our blog