The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide

/ 1 3 3

UFALME WA MUNGU

Maangamizi au Hukumu ya Milele?

Katika mahubiri yenye nguvu kuhusu dhambi, msamaha, na upatanisho, mchungaji wa kanisa fulani anadai kwamba haamini tena kwamba hukumu ni ya milele, yaani, kwamba waliopotea watateswa milele na milele. Ingawa ana hakika kwamba hukumu ya Mungu itakuwa ya mwisho, na kwamba ni wale tu wanaomwamini Kristo wataishi katika Ufalme wa milele wa Mungu, yeye anashikilia msimamo kwamba nukuu zote katika Biblia kuhusu hukumu ya milele ya waliopotea si kwamba watu watateswa milele, bali ni kwamba hukumu yao haitaweza kupinduliwa milele. Sasa anaamini kwamba waliopotea wataangamizwa, hawatarudi tena duniani au kufurahia baraka za Mungu. Huu unaoitwa «mtazamo mpya» umesumbua wengi kanisani, na hata baadhi ya wazee wanafikiria kuitisha mkutano maalum ili kushughulikia mtazamo wa mchungaji kuhusu kuzimu. Kanisa linapaswa kufanya nini sasa na mtazamo mpya wa mchungaji wao kuhusu hukumu ya milele? Umeombwa utoe neno la wasifu kwenye mazishi ya mtu mpendwa kazini, ambaye familia yake inakujua kuwa mhudumu, au angalau, “mtu wa dini.” Kutokana na mazungumzo na marehemu, una uhakika kabisa kwamba hakumjua Bwana; kwa hakika, katika mazungumzo ya mwisho mliyozungumza naye kuhusu Bwana, aliitikia kwa chuki na hasira kali. Wana-familia wanatumai unaweza kuwapa maneno ya kufariji kuhusu mpendwa wao katika ibada hiyo. Je, kwa kuzingatia yale unayofahamu kuhusu kukamilishwa kwa Ufalme, unaamini unapaswa kuzungumza nini kama “neno la Bwana” kwa familia ya dada huyu mpendwa? Ufalme wa Mungu utakamilika katika Ujio wa Pili wa Yesu Kristo. Eskatolojia, somo la mambo ya mwisho, inashughulika na dhana ya utimilifu wa Ufalme. Kukamilishwa kwa Ufalme wa Mungu kutatokea katika Ujio wa Pili wa Yesu Kristo, ambaye hivi karibuni atafunuliwa na atasimamisha utawala wake duniani. Parousia ni neno linalohusishwa na kurudi kwa Yesu, tendo ambalo litakuwa la kibinafsi, katika mwili, linaloonekana, la utukufu, na la upesi. Kukamilishwa huko kwa Ufalme kunafungamana kabisa na yale ambayo Biblia inafundisha kuhusu kifo, ufufuo, na hukumu ya mwisho. Maadui wote watakapowekwa chini ya miguu ya Yesu, atakabidhi Ufalme kwa Mungu Baba yake ili Mungu awe Yote katika yote. Neno Sahihi kwa Wakati Ufaao

2

3

4

Marudio ya Tasnifu ya Somo

Made with FlippingBook Learn more on our blog