The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide

/ 1 5

UFALME WA MUNGU

Kupingwa kwa Utawala wa Mungu

SOMO LA 1

ukurasa 307  1

Karibu katika Jina lenye nguvu la Yesu Kristo! Baada ya kusoma, kujifunza, kushiriki katika mijadala, na kutendea kazi yaliyomo katika somo hili, utakuwa na uwezo wa: • Kueleza jinsi Mungu kama Bwana, anavyotawala juu ya vyote, lakini kwamba utawala wake ulipingwa kupitia uasi wa kishetani huko mbinguni, na kupitia uasi wa hiari na kutotii kwa wenzi wa kwanza wa kibinadamu duniani. • Kuonyesha jinsi uasi huu ulivyosababisha laana juu ya uumbaji, iliyopelekea kifo, na maafa makubwa zaidi ya wanadamu wote, jambo ambalo Kanisa huliita “Anguko.” • Kuonyesha namna ambavyo kutotii huku kwa Shetani na wanadamu wawili wa kwanza kumeleta matokeo yenye kuhuzunisha na ya uharibifu katika nyanja tatu za uhai na maisha katika uumbaji: kosmos (ulimwengu), sarx (mwili wa asili ya mwanadamu), na kakos (ushawishi unaoendelea na machafuko ya yule mwovu). • Kukariri kwa moyo kifungu kinachohusiana na kupingwa kwa utawala wa Mungu. Soma Zaburi 2:1-12. Je, Mungu anacheka? Katika mojawapo ya maandiko ya kustaajabisha zaidi katika Maandiko Matakatifu, tunasoma hapa kuhusu nia ya mataifa ya kupinga utawala wa Bwana na Mpakwa-Mafuta wake. Kwa kuitikia jaribio hili lisilo na maana la mataifa la kujitenga na utawala wa ufalme wa Mungu, mtunga-zaburi anadokeza kwamba Bwana atazicheka jitihada zao ndogo na duni za kupinga utawala wake. Kwa hakika, Bwana anathibitisha kwamba amemweka Mfalme wake juu ya Sayuni, mlima wake mtakatifu, na kwamba Mwanawe atatawala bila kupingwa akiwa Bwana wa wote. Mpakwa-Mafuta wa BWANA atamiliki mataifa hadi miisho ya dunia, na kuyavunja-vunja mataifa hayo yenye upinzani kama mitungi ya udongo. Mtunga-zaburi anamalizia maono haya makuu kwa kusihi wafalme wa dunia wawe na utambuzi na kupokea onyo. Imewapasa kumwabudu BWANA, kama Mfalme juu ya vyote, na kumsujudia Mwana kwa Utawala wa Mpakwa Mafuta wa BWANA

Malengo ya Somo

ukurasa 307  2

1

Ibada

ukurasa 307  3

Made with FlippingBook Learn more on our blog