The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide
1 6 /
UFALME WA MUNGU
kumbusu miguu yake, ili ghadhabu na hasira yake isije ikaachiliwa, wakaangamizwa katika ghadhabu yake kuu. Hebu tukubaliane kwa moyo wote na mtunga-zaburi katika mstari wa 12: «Heri wote wanaomkimbilia» (Zab. 2:12).
Baada ya kutamka na/au kuimba Kanuni ya Imani ya Nikea (katika kiambatisho), sali sala ifuatayo: Mungu wa Milele, Baba yetu, tunakushukuru kwamba wewe peke yako ndiwe Mungu, unayetawala juu zaidi ya mbingu na nchi kama Bwana Mungu Mwenye Enzi Kuu. Ijapokuwa utawala wako wa haki ulipingwa na malaika na wanadamu, umerejesha utawala wako kupitia Mwanao, na hivi karibuni utafanya vitu vyote hapa duniani kama vile mbinguni – sawa sawa na mapenzi yako matakatifu na mema. Utukuzwe kupitia sisi tunapoishi kwa kudhihirisha utawala wako wa haki katikati ya watu wako, Kanisa, kama ushuhuda kwa jamii zetu na ulimwengu wetu. Katika jina la Yesu, Amina.
Kanuni ya Imani ya Nikea na Maombi
ukurasa 307 4
1
Hakuna jaribio kwa somo hili
Jaribio
Mazoezi ya Kukariri Maandiko
Hakuna Maandiko ya kukariri katika somo hili
Hakuna kazi za kukusanya katika somo hili
Kazi za Kukusanya
MIFANO YA REJEA
Ulimwengu Ulioshindikana
Hebu fikiria unazungumza na mmoja wa majirani zako kuhusu hali ya sasa ya jamii na ulimwengu. Ungemjibuje jirani yako ikiwa angetoa kauli ifuatayo: “Kutokana na kila kitu ninachoona katika jamii, na kutokana na matukio haya yote katika ulimwengu, nadhani kwamba Mungu, kama kweli yeye ni halisi, basi ni ama hana udhibiti juu ya ulimwengu, au hawezi kukabiliana na kiwango cha uovu uliomo. Kila kitu kinaharibika. Haiwezekani Mungu akawa na udhibiti – ulimwengu umeharibika sana!” Je kauli hii inaendana na mawazo yako? Kwa nini ndiyo au kwa nini hapana? Unawezaje kumjibu mtu ambaye ana maoni ya namna hii kuhusu ulimwengu wetu leo?
1
ukurasa 308 5
Made with FlippingBook Learn more on our blog