The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide

/ 1 7

UFALME WA MUNGU

Ushahidi wa Utawala wa Mungu Duniani

Ingawa Biblia inafundisha kwamba Mungu ni Mweza wa Yote, inaonekana kwamba ulimwengu haujui kabisa nguvu na utukufu wake. Toa sababu tano zinazofanya kuwe na mantiki kusema kwamba ingawa ulimwengu unateseka kutokana na ukosefu wa haki, uonevu, na jeuri, Mungu angali ni Mungu Mweza wa Yote, mwenye uwezo na mamlaka yote, na anayedhibiti kila kitu.

2

Ikiwa Kweli Mungu Anatupenda. . .

Pata picha kwamba umeitwa kwenye nyumba ya familia moja pendwa ambayo kijana wao aliuawa hivi majuzi wakati wa tukio la ufyatulianaji wa risasi usio na sababu wa magenge ya uhalifu. Unapokuwa hapo ukisaidia kuifariji familia, mmoja wa wana familia anasema mbele ya wote waliopo, “Ukweli kwamba jambo hili lilitukia unaonyesha kwamba Mungu hatupendi kiukweli. Ikiwa kweli Mungu anatupenda, mambo ya aina hii yasingetokea kamwe. Mungu mwema angewezaje kuruhusu mambo ya aina hii yatendeke kwa kijana mdogo na asiye na hatia?” Je, jibu lako litakuwa nini kwake na kwa wengine waliosikia maoni haya kutokana na mkasa huo?

1

3

Kupingwa kwa Utawala wa Mungu Sehemu ya 1

YALIYOMO

Mch. Dkt. Don. L. Davis

Mungu, kama Bwana, anatawala juu ya vyote, lakini utawala wake ulipingwa kupitia uasi wa kishetani huko mbinguni, na kupitia uasi wa hiari na kutotii kwa wanadamu wawili wa kwanza duniani. Upinzani huu ulisababisha laana juu ya uumbaji, iliyopelekea kifo, na tatizo kubwa zaidi ya maafa yote yanayowakumba wanadamu. Kanisa linaita tatizo hilo “Anguko.” Kusudi letu katika sehemu hii ya kwanza ya Kupingwa kwa Utawala wa Mungu ni kukuwezesha kuona kwamba: • Mungu ndiye Mwenye Enzi Kuu juu ya ulimwengu wote. • Ubwana wake ulipingwa, na ibilisi na malaika zake, na wanadamu wawili wa kwanza, Adamu na Hawa, kupitia kutotii kwao kimakusudi katika bustani.

Muhtasari wa Sehemu ya 1

ukurasa 308  6

Made with FlippingBook Learn more on our blog