The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide
6 /
UFALME WA MUNGU
Kanisa lake. Kanisa la Yesu Kristo ni kituo cha—mahali pa au muktadha wa— wokovu wa Mungu, ni mahala pa uwepo unaotia nguvu wa Roho Mtakatifu, kituo cha shalom halisi ya ufalme, mahali ambapo uwepo na nguvu za Mungu zinadhihirishwa kwa uhuru. Utawala wa ufalme wa Mungu utakamilika katika Ujio wa Pili wa Yesu, ambapo kifo, magonjwa, na uovu wote vitawekwa chini, mbingu zote na dunia zitafanywa upya, na Mungu atakuwa Yote katika yote. Hadithi ya Ufalme ni hadithi ya Yesu, na nia ya Mungu ni kurejesha ulimwengu chini ya utawala wake kwa njia ya Kristo. Ombi letu ni kwamba upendo na utumishi wako kwake uongezeke kwa wingi unapojifunza Neno la Mungu kuhusu utawala wa milele wa Mungu! Tunamsifu Mungu kwa hadithi yake ya ufalme, na kwa ajili ya shauku yako kama mwanafunzi wa Neno lake Takatifu!
- Mchungaji Dkt. Don. L. Davis
Made with FlippingBook Learn more on our blog