The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide
/ 7 1
UFALME WA MUNGU
la aina fulani, si lazima kabisa kujihusisha kwa ukaribu katika kanisa ili kuwa wa kiroho. Maadamu moyo wa mtu uko wazi, amejitoa kwa Kristo na kwa Maandiko, na anadumisha “ukaribu” na Mungu, basi kila kitu kiko sawa. Au unasemaje?
Kuchukulia Mambo Mbali Kidogo
Unafikiri nini kuhusu mafundisho ya sasa ya injili ya “utajiri-afya”? Fundisho hili, kwa maelezo rahisi, linakazia kwamba kwa sababu mkristo amekuwa chini ya serikali na mamlaka ya Mwenyezi Mungu, kwamba sasa hakuna haja ya mwamini kuwa mgonjwa, mhitaji, au maskini. Kiini cha hili, kulingana na fundisho lenyewe, kinatokana na mamlaka ya mkristo. Yesu alipopaa mbinguni, inadaiwa kwamba kwa sababu Yesu alikuwa na mamlaka yote, na kwa sababu alikabidhi mamlaka hayo kwa watu wake, yaani Kanisa, basi Kanisa linaweza kutawala moja kwa moja juu ya shetani, na kuzuia nia yake ya kulidhuru au kuliumiza Kanisa. Kwa hakika, wengine wanaoshikilia fundisho hili wanaamini kwamba ikiwa wewe ni mgonjwa au ni mhitaji au umepitia hali ya kushindwa katika maeneo fulani ya maisha, ni kosa lako mwenyewe. Mungu amekupa neema, na unachohitaji kufanya ni kuithibitisha. Je, hii ni sahihi au ni kuchukulia mambo mbali kidogo? Mojawapo ya masuala yanayokinzana na yenye matatizo katika historia ya Kanisa linaweza kuwekwa katika mfumo wa swali: Uhusiano wa Kanisa na ulimwengu unapaswa kuwa upi? Je, tunapaswa kufikiria vipi kuhusu uhusiano wa Kanisa na ulimwengu? Je, ni lugha nzuri kuzungumza juu ya Kanisa kuvamia malango ya kuzimu, au je, Kanisa litoke miongoni mwao na kutengwa nao? Kusema kweli, ni kielelezo gani bora zaidi cha kuelewa uhusiano wa Kanisa na ulimwengu – Je, Kanisa linapaswa kutafuta kubadilisha ulimwengu, Kanisa lijiondoe ulimwenguni, au Kanisa liishi katika mvutano na ulimwengu kwa namna fulani? Kielelezo Gani ni Bora Zaidi?
2
3
3
Made with FlippingBook Learn more on our blog