The Kingdom of God, Swahili Student Workbook
/ 1 9
UFALME WA MUNGU
C. Ukuu wa Mungu umekita mizizi katika nafsi yake, na kudhihirishwa katika kazi zake zote. Dk. Lewis Chafer, mwanzilishi wa Seminari ya Dallas, na Dk. Walvoord, katika kuzungumza juu ya ukuu wa Mungu wanaeleza: . . . sifa za Mungu zinaweka wazi kwamba Mungu ni mkuu juu ya vyote. Hajitiishi chini ya nguvu nyingine, mamlaka nyingine au utukufu mwingine, na hayuko chini ya yeyote kwa kuwa hakuna aliye mkuu kuliko Yeye mwenyewe. Anawakilisha ukamilifu kwa kiwango kisicho na kikomo katika kila kipengele cha uwepo wake. Hawezi kamwe kushangaa, kushindwa, au kutokuwa na uhakika. Hata hivyo, bila kudhabihu mamlaka yake au kuhatarisha utimilifu wa mwisho wa mapenzi yake makamilifu, imempendeza Mungu kuwapa [wanadamu] {watu} kiasi cha uhuru wa kuchagua, na kwa ajili ya utekelezaji wa uchaguzi huo Mungu huwawajibisha [wanadamu] {watu}. Lewis Sperry Chafer na John Walvoord. Major Bible Themes . Grand Rapids: Zondervan, 1975. uk. 42.
1
1. Danieli 4:34-35
2. Bwana ni Mungu, Mungu mkamilifu asiye na kikomo, ambaye anastahili ibada na utii wetu.
3. Utawala wa Mungu umepingwa.
a. Na adui mkuu wa wanadamu, Ibilisi
b. Na wanandoa wa kwanza wa kibinadamu
II. Uasi wa Ibilisi (Shetani) mbinguni unawakilisha upinzani wa kwanza na mbaya zaidi kwa Enzi Kuu ya Mungu katika Ulimwengu.
A. Maelezo ya Agano la Kale ya Shetani kama Lusifa, Mwana wa Asubuhi
Made with FlippingBook - Online catalogs