Theology of the Church, Swahili Mentor Guide
1 6 /
THEOLOJIA YA KANISA
rehema, bali sasa mmepata rehema.” Kanisa ni watu waliochaguliwa na Mungu, makuhani wake wanaomwabudu, na kati ya mataifa yote, Kanisa sasa ni taifa la Mungu linaloishi duniani kulingana na maadili ya Ufalme wa Mungu. Jukumu letu ni kuishi kwa namna ambayo yeyote anayetaka kujua jinsi dunia inayoongozwa na Mungu inavyoonekana, anaweza kujua kwa kuliangalia Kanisa. Huu ni upendeleo wa ajabu na wito wa hali ya juu. Baada ya kukiri na/au kuimba Kanuni ya Imani ya Nikea (iliyopo kwenye viambatisho), omba maombi yafuatayo: Mungu wa Ibrahimu, Isaka, na Yakobo, asante sana kwa kutujumuisha sisi sote tuliomwamini Yesu kama watoto wa Ibrahimu na warithi wa ahadi ulizompa. Baba, tusaidie kukuwakilisha vyema katika dunia hii ya dhambi. Tusaidie kuwa tofauti na mataifa yanayotuzunguka ili tuangaze kama mji ulioko juu ya mlima. Tusaidie kufanya matendo mema yanayowawezesha watu kuuelewa moyo wako na kukutukuza wewe, Baba yetu wa mbinguni. Na zaidi ya yote, tusaidie kutangaza kwa ujasiri habari njema za Yesu ili kila mtu apate fursa ya kuwa miongoni mwa watu wako uliowachagua. Tunaomba haya kupitia Yesu Kristo Bwana wetu, anayemiliki pamoja nawe na Roho Mtakatifu, Mungu mmoja, milele na milele. Amina.
Kanuni ya Imani ya Nikea na maombi
1
ukurasa 218 4
Hakuna jaribio katika somo hili.
Jaribio
Hakuna Maandiko ya kukariri katika somo hili.
Mapitio ya Kukariri Maandiko
Hakuna kazi za kukabidhi katika somo hili.
Kazi za Kukabidhi
MIFANO YA REJEA
Muda Mwingi Umetumika kwa ajili ya Wakati Ujao
Baada ya semina ambayo mchungaji alikuwa akifundisha kuhusu siku za mwisho, mmoja wa waamini alitoa maoni baadaye katika maegesho ya magari, akisema: “Sielewi kabisa kwa nini tunahitaji kutumia muda mwingi sana kuzungumzia mambo ya ile picha kubwa. Hii ndiyo sababu Kanisa linachosha watu wengi – hatujui jinsi ya kuwekea mkazo mambo yanayotokea leo. Kila kitu ni ndoto
1
ukurasa 219 5
Made with FlippingBook - Share PDF online