Theology of the Church, Swahili Mentor Guide

/ 1 7

THEOLOJIA YA KANISA

za mbinguni, paradiso ya siku za baadaye, kusudi fulani la kiungu kuhusu kile ambacho Mungu atafanya siku moja. Sielewi kwa nini tunapaswa kila mara kuzungumzia mambo haya ya ile picha kubwa. Ninahitaji kujikita katika kile ninachopaswa kufanya leo!” Je, ungemjibuje muumini aliyelemewa kwa njia hii?

Utambulisho

Chukua kipande cha karatasi na chora seti ya alama au picha ndogo ambazo zingemsaidia mtu asiyejua chochote kuhusu wewe apate kuelewa wewe ni nani na ni mambo gani yanayokushughulisha. Kisha fuata maelekezo ambayo Mkufunzi wako atakupa kabla ya kuwaonyesha wengine picha hizo.

2

ukurasa 219  6

1

Waliokolewa na Waliopotea

Maandiko yanazungumza mara nyingi juu ya watu “waliokolewa” na “waliopotea.” Kwa mtu ambaye hajawahi kusikia Injili, lugha hii inaweza kuwa ngumu kuelewa. Maswali ya msingi yanayoweza kujitokeza ni: “Tumeokolewa dhidi ya nini?” na “Unamaanisha nini unaposema kuwa nimepotea?” Je, ungemjibuje mtu anayekuuliza maswali haya?

3

Ufunuo Kivuli wa Kanisa katika Mpango wa Mungu Sehemu ya 1

YALIYOMO

Mchungaji Dkt. Don L. Davis

Kanisa limefunuliwa kwa namna ya kivuli katika mpango wa Mungu uliotukuka kwa ajili yake mwenyewe; amekusudia kujitukuza mwenyewe kwa kuwakomboa wanadamu wapya kupitia agano ambalo alifanya na Ibrahimu. Limefunuliwa pia katika mchakato wa kufunuliwa kwa mpango wake wa neema ya wokovu, ambao unajumuisha kusudi la ajabu la kuwahusisha mataifa katika makusudi yake ya Ufalme. Hatimaye, Kanisa limetabiriwa katika picha iliyofunuliwa na Maandiko ya Mungu ya kuumba kwa ajili yake watu wa kipekee, yaani laos wa Mungu.

Muhtasari wa Sehemu ya 1

Made with FlippingBook - Share PDF online