Theology of the Church, Swahili Mentor Guide

1 8 /

THEOLOJIA YA KANISA

Lengo letu katika sehemu hii ya kwanza ya Ufunuo Kivuli wa Kanisa katika Mpango wa Mungu ni kukuwezesha kuona kwamba: • Kanisa lilifunuliwa tangu awali katika kusudi kuu la Mungu la kujitukuza mwenyewe kupitia jamii mpya ya wanadamu watakaoishi pamoja naye milele. • Kanisa lilifunuliwa awali katika ahadi ya Mungu ya kuwajumuisha Wamataifa katika mpango wake wa ukombozi kwa ulimwengu. • Kanisa lilifunuliwa awali katika jitihada za Mungu za kujitengenezea watu ( laos ) watakaoishi kwa ajili yake kama watu wake wa pekee. • Mungu anafanya kazi kupitia historia ya wanadamu ili kujichagulia watu wake kutoka katika mataifa yote duniani.

1

I. Kanisa la Yesu Kristo lilifunuliwa awali katika mpango wa Mungu uliotukuka: Kujiletea utukufu kupitia jamii mpya ya wanadamu, kulingana na tangazo la awali la Injili katika Agano na Ibrahimu.

Muhtasari wa Sehemu ya Kwanza ya Video

ukurasa 219  7

A. Kusudi kuu la Mungu ni kuliletea heshima Jina lake.

1. Uumbaji wote ulifanyika kwa mapenzi yake na kwa nguvu zake, na kwa ajili ya utukufu wake.

a. Kut. 20:11

b. Isa. 40:26-28

c. Yer. 32:17

2. Mwandishi wa Zaburi anasema kwamba ilikuwa kwa utukufu wake Mungu alipochagua na kutekeleza mpango wake wa ukombozi kwa watu wake Israeli na kuwashinda adui zake katika mpango wake, Zab. 135:8-12.

Made with FlippingBook - Share PDF online