Theology of the Church, Swahili Mentor Guide

/ 2 7

THEOLOJIA YA KANISA

B. Kutengwa na Mungu kulikosababishwa na dhambi kunamaanisha kwamba wanadamu wamepotea. Wanadamu hawapo tena pale wanapopaswa kuwa, bali wamepotoka mbali na Mungu kama kondoo waliopotea. Katika Luka 15, Yesu alielezea hali ya mwanadamu iliyosababishwa na dhambi kwa kutumia dhana ya upotevu kabisa. Anasimulia hadithi zinazoonyesha kwamba wanadamu ni kama:

1. Mwana aliyepotea

1

2. Kondoo aliyepotea

3. Sarafu iliyopotea

Luka 19:10 Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kilichopotea.

C. Matokeo matatu ya kutengwa na Mungu ni Kifo, Utumwa, na Hukumu.

1. Kwa kuwa Mungu ndiye chanzo cha uzima wote, upotevu/kutengwa kunakosababishwa na dhambi kumeleta matokeo ya kifo, kama inavyoonyeshwa wazi katika kisa cha Adamu na Hawa.

a. Mwa. 2:16-17

b. Luka 15:24

c. Ona pia Warumi 5:12, Efe. 2:1

2. Kwa kuwa Mungu ndiye chanzo cha uhuru na ulinzi, upotevu/ kutengwa kwetu naye kumesababisha utumwa wetu chini ya dhambi na shetani.

Made with FlippingBook - Share PDF online