Theology of the Church, Swahili Mentor Guide
/ 2 9
THEOLOJIA YA KANISA
B. Umoja na Kristo una kipengele cha kisheria (kimahakama): Mungu aliweka hasira na hukumu yake juu ya Kristo ambaye alikufa badala yetu. Kupitia umoja na Kristo, tunashiriki katika kifo chake msalabani na hivyo, Mungu anazitambua dhambi zetu kuwa zimelipiwa gharama, na kwa neema anazisamehe.
ukurasa 224 13
1. Isa. 53:5
2. Ebr. 9:28
1
3. Kol. 2:13-14
Kwa kuwa imani ni tendo la kuamini katika Kristo na kuwa umoja na Kristo, huku kuhesabiwa haki si ujanja au kujifanya, kana kwamba Mungu anatangaza kuhusu sisi jambo ambalo halipo. Badala yake, kwa sababu ya umoja wetu na Kristo kwa njia ya imani (na kwa njia hiyo Kristo akiwa ndani yetu), Mungu anatangaza kile kilicho kweli. Ndiyo, Mungu anawehasabia haki wasiokuwa na haki, lakini ni pale tu wanapokuwa waamini katika Kristo na hivyo wameunganishwa na Yeye. Hivyo basi, mwenye dhambi anavikwa haki ya Kristo na kwa namna fulani anajulikana kuwa mwenye haki, lakini hili linatokea kwa njia ya imani inayomuunganisha mtu na Yesu Kristo... Hii haimanishi kwamba sisi si wenye dhambi tena, maana kwa kweli ndani yetu wenyewe sisi ni wenye dhambi. Lakini katika Kristo, sisi ni wenye haki kabisa! ~ J. Rodman Williams. Renewal Theology . Toleo la 2. Grand Rapids: Zondervan, 1996. uk. 74.
C. Umoja na Kristo una kipengele cha kiroho: Kwa sababu roho zetu zimeunganishwa na Roho wake, maisha ya Yesu yanatiririka kupitia kwetu na kutushindia dhidi ya ufisadi na kifo.
1. Rum. 8:10-11
2. Kol. 3:3-4
Made with FlippingBook - Share PDF online