Theology of the Church, Swahili Mentor Guide
/ 3 3
THEOLOJIA YA KANISA
Hivyo, Mungu siyo tu anawaokoa watu binafsi na kuwaandaa kwa ajili ya kwenda mbinguni; bali anaunda watu kwa ajili ya Jina lake, ambao Mungu anaweza kukaa kati yao na ambao katika maisha yao pamoja wataakisi maisha na tabia ya Mungu. Mtazamo huu wa wokovu ni wa kina kwa Paulo. ~ Gordon D. Fee. God’s Empowering Presence . Peabody: Hendrickson, 1994. uk. 872.
D. Maandiko ya Agano la Kale yalijenga msingi wa kuelewa kwamba wokovu ni kuunganishwa na watu wa Mungu.
ukurasa 224 14
1
1. Wokovu kutoka Misri (Kutoka):
Labda picha bora kabisa ya wokovu katika Biblia ni hadithi ya Kutoka ambapo wana wa Israeli wanakombolewa kutoka utumwani nchini Misri. Tangu enzi za awali katika historia ya Kanisa, hadithi ya Kutoka ilieleweka kama hadithi inayofafanua ufahamu wa Kikristo wa wokovu. Angalia jinsi hadithi ya Kutoka
a. Watu watumwa wanaoishi katika mateso bila matumaini (Waisraeli katika Misri),
b. Wanaitwa na Mungu kwa uchaguzi wake wa neema kupitia shujaa ambaye Mungu anamtuma (Musa),
c. Wanaokolewa na ghadhabu ya Mungu kwa njia ya damu (Mwana kondoo wa Pasaka),
inavyotoa taswira ya maana halisi ya kuokolewa.
d. Wanaokolewa kutoka kwa mfalme mwovu kupitia nguvu kuu za Mungu (ushindi dhidi ya Farao na majeshi yake),
e. Wanakombolewa kwa kupita katika maji (Bahari ya Shamu),
f. Wanaundwa kuwa taifa takatifu (Israeli) wanaotii mapenzi ya Mungu (Torati),
g. Wanapewa jukumu la kuwa mashahidi kwa mataifa (Kutoka 19:5-6),
Made with FlippingBook - Share PDF online