Theology of the Church, Swahili Student Workbook
/ 2 5
THEOLOJIA YA KANISA
6. Mitume walihusianishaje ahadi ya Mungu kwa Israeli na Kanisa la Mungu katika Kristo Yesu? Toa mifano. 7. Kanisa kupitia Kristo limepewa nafasi maalum katika mpango wa wokovu wa Mungu. Sasa, basi, Israeli ina nafasi gani kama watu wa Mungu? Je, Mungu ameiacha Israeli au kufuta uteuzi wake? Eleza.
Ufunuo Kivuli wa Kanisa katika Mpango wa Mungu Sehemu ya 2: Wokovu: Kujiunga na Watu wa Mungu
1
Mch. Terry Cornett
Kwa sababu ya dhambi, kila mwanadamu yuko katika hali inayoweza kuonekana kuwa ya kukata tamaa. Tunahitaji kuokolewa kwa haraka kutoka katika dhambi na madhara yake, lakini asili yetu ya dhambi inatufanya tusitamani wokovu wa Mungu wala kuwa na njia yoyote ya kurudishwa kwake. Cha kushangaza, Mungu alikataa kutuacha kama maadui wake. Mtume Paulo anafundisha kwamba ingawa tulikuwa tumefungiwa katika dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu. Injili ni habari njema kwamba Mungu ametoa neema ya wokovu ambayo inaweza kutufanyia yale ambayo hatuwezi kuyafanya sisi wenyewe. Kuelewa neema hii ndiyo msingi wa kutambua jukumu la Kanisa kama jamii ya waabudu. Lengo letu kwa ajili ya sehemu hii, Wokovu: Kujiunga na Watu wa Mungu , ni kukuwezesha: • Kutoa tafsiri ya kitheolojia ya wokovu. • Kuelezea madhara ya kutengwa na Mungu. • Kueleza faida zinazokuja kwetu kupitia umoja wetu na Kristo. • Kuelewa jinsi tendo la Kutoka ( Exodus ) linavyotumika kama (kivuli) mfano wa wokovu katika Kikristo. • Kuelewa kwamba kuingizwa katika Kanisa (watu wa Mungu) si kitu cha ziada kinachoongezwa baada ya wokovu bali ni jambo muhimu katika maana ya msingi kuokolewa.
Muhtasari wa Sehemu ya Pili
Made with FlippingBook flipbook maker