Theolojia Katika Picha

1 1 0 /

R e p r e s e n t a n d o l a t e o l o g í a

Kikosi cha Kitume Kukuza Ufikiaji kwa ajili ya Ufanisi katika Mavuno Mch. Dkt. Don L. Davis

Walengwa: Wakazi Wazungu Maskini wa Jamii fulani

Makambi na makazi ya muda

Klabu za Vijana

• Hutazama timu ya upandaji makanisa kama kikundi thabiti chenye uwezo wa kubadilika kuendana na mazingira. • Sehemu ya kuhubiri inachukuliwa kama wavu wa kuvulia samaki . • Kuzingatia ujuzi, vipawa na uwezo uliothibitishwa . • Huruhusu shughuli na miradi ya dharura . • Kiongozi wa Timu hutumia sehemu mbalimbali za mahubiri kuitambulisha kampeni . • Hutafuta kutumia karama tano za Waefeso 4. • Huzingatia kutafuta mwitikio si shughuli . • Hufanya kazi kwa kuzunguka maeneo mbali mbali . • Husumbuliwa na vizuizi vya muda, rasilimali, na upokeaji. • Hufanya kazi kupitia wanafunzi, si wamishenari. • Huunganisha ibada, kufuasa na uongozi . • Hufanya kazi kwa kanuni, imani na itifaki za pamoja . • Hutafuta kupanda makanisa kwa wingi na kwa umoja .

Eneo la Mahubiri 1

Eneo la Mahubiri 6

Chumba cha Urembo

Jengo la wapangaji

Eneo la Mahubiri 2

Eneo la Mahubiri 5

Kumbi za mchezo wa Bowling

Maeneo ya kuogelea

Eneo la Mahubiri 4

Eneo la Mahubiri 3

Dhana za Msingi 1.  Kuzunguka – Kikosi cha Kitume hufanya kazi katika maeneo na miktadha mingi kwa wakati mmoja kwa lengo la pamoja la kufikia jamii funali inayolengwa. 2.  Umoja – Kikosi cha Kitume hutumia mifumo, mbinu, na itifaki zinazofanana kuvuna na kuwajenga waongofu. 3.  Mamlaka – Kikosi cha Kitume hufanya kazi chini ya muundo wa mamlaka na msingi wa kiuongozi wa pamoja. 4.  Utambulisho – Kikosi cha Kitume hupanda makanisa ya aina moja yenye mafundisho, utendaji, miundo na mila ya pamoja. 5.  Karama – Kikosi cha Kitume hutenda kazi kwa kuzingatia karama zilizo thibitishwa za kikundi, sio upatikanaji na uwajibikaji pekee. 6.  Ufanisi – Kikosi cha Kitume huwekeza kwa watu wanaoitikia katika sehemu za mahubiri, kwa kuwapa wale wanaopokea uangalifu wa kutosha na muhimu. 7.  Uratibu – Kikosi cha Kitume huandaa na kutumia watu waliochaguliwa ili kutoa mchango wao katika nyakati muhimu kwa ajili ya shughuli mahususi. 8.  Uimarishaji – Kikosi cha Kitume huimarisha matokeo katika eneo fulani kwa lengo la kuanzisha na kukuza vuguvugu (harakati) na kuleta maongezeko, na sio kudumu hapo. 9.  Nidhamu – Kikosi cha Kitume hufanya kazi kulingana na utaratibu na muundo mahususi, ili kuwaandaa wanafunzi katika nidhamu za imani. 10.  Uanzilishi – Kikosi cha Kitume hutafuta kuzindua na kuanzisha uzazi na malezi ya kiroho, na kukabidhi sehemu kubwa ya ukuaji na ukomavu wa kusanyiko kwa uangalizi wa kichungaji.

U F A F A N U Z I W A M A N E N O :

Kikosi cha Kitume - timu thabiti ya watendakazi wenye vipawa, wanaopatikana, na waliojitolea ambao wamepewa kufanya jukumu fulani au kutekeleza kazi maalum zinazochangia kuifikia jamii fulani ya watu. Sehemu ya Mahubiri - eneo, ukumbi, au mahali mahususi ambapo watu wa jamii lengwa wanaishi au kukusanyika. Mkataba wa Timu - makubaliano ya msingi yanayotegemea muda na rasilimali zinazohitajika ili kufikisha Injili kwa uaminifu kwa watu wanaolengwa katika eneo fulani. Usimamizi wa Miradi - kuweka pamoja kundi la muda la watu, mikakati, na rasilimali ili kukamilisha kazi, ufikiaji, au tukio fulani.

Made with FlippingBook Digital Publishing Software