Theolojia Katika Picha

/ 1 6 7

R e p r e s e n t a n d o l a t e o l o g í a

Kuunda Harakati Madhubuti za Kupanda Makanisa Mijini Kutambua Sifa za Jumuiya Halisi ya Kikristo ya Mijini Mch. Dkt. Don L. Davis

t i

a

r

b

a

u

T

Misingi ya Kiinjili

z

a

a

n

P a

a

i k

m

i r

o j

S h

a

Mduara huu unawakilisha misimamo na nyajibu zake za msingi zaidi , uthibitisho wake wa Imani, kujiweka kwake wakfu kwa ajili ya Injili na kweli zile zilizomo katika kanuni za imani za Kikristo za kale (yaani, Kanuni ya Imani ya Nikea). Misimano hii imejikita katika imani yake katika Neno la Mungu, na inawakilisha uaminifu wetu kwa usahihi wa kihistoria. Kama washiriki wa Mwili mmoja, mtakatifu, wa kitume na wa kikatoliki (wa ulimwengu) wa Kristo, harakati lazima ziwe tayari na radhi kufa kwa ajili ya misingi yao mikuu ya kiinjili . Misingi hii hutumika kama kiunganishi cha mienendo na imani ya kihistoria ya Kikristo, na kwa sababu hiyo, kamwe haiwezi kukengeushwa au kubadilishwa.

o

B

z a

h

a i

a

s

i

n i

u l

s

b

w

h

H

i

m

w

o

a

u d

t

a

n d

U

u

K

a

u u

a

a

m a

y

i

K

n

g

i

n

i

n

n

i

i

i s

t i

j

s

i

M

M i

l

a

i

U

Harakati za Kupanda Makanisa Mijini

Utii na Utambulisho Bainishi wa Kanisa

Mduara huu unawakilisha utii na utambulisho wao bainishi . Harakati za Kupanda Makanisa ya mijini zitaungana kwa kuzingatia mila zao bainifu, zikisimamiwa na viongozi wanaozipatia harakati hizo maono, mafundisho, na mwelekeo wanaposonga mbele pamoja ili kumwakilisha Kristo na Ufalme wake katikati ya majiji. Mapokeo mahususi hutafuta kueleza na kuuishi uaminifu huu kwa Mapokeo Yenye Mamlaka na na Mapokeo Makuu kupitia ibada, mafundisho, na huduma zao. Mapokeo mahususi hutafuta kuifanya Injili iweze kueleweka ndani ya tamaduni mpya au tamaduni ndogo, kwa kuzungumza na kutoa kielelezo cha tumaini la Kristo katika hali mpya zinazoundwa na maswali yao wenyewe yanayoulizwa kulingana na hali zao mahususi. Kwa hiyo, harakati hizi zinatafuta kuweka muktadha wa Mapokeo Yenye Mamlaka kwa namna ambayo, kwa uaminifu na ufanisi, yataongoza vikundi vipya vya watu kwenye imani katika Yesu Kristo, na kuwaingiza wale wanaoamini katika jumuiya ya imani inayotii mafundisho yake na kuwashirikisha wengine ushuhuda wake.

Harakati za Kupanda Makanisa mijini lazima ziwe tayari na radhi kueleza na kutetea tofauti zao bainifu kama jumuiya ya ufalme wa Mungu mjini.

Muundo wa Shirika na Taratibu za Pamoja za Huduma

Mduara huu unawakilisha njia ambazo harakati za Kupanda Makanisa ya mjini zinaakisi imani na utambulisho wao kupitia miundo yao tofauti ya kishirika na taratibu za huduma . Miundo na taratibu hizi zinaundwa na kutekelezwa kupitia mikakati, sera, maamuzi na taratibu zao mahususi. Miundo na taratibu zinawakilisha mbinu walizochagua wenyewe za kudhihirisha uelewa wao wa imani kama inavyohusiana na madhumuni na utume wao kama jumuiya. Miundo na taratibu hizi zinaweza kubadilika kupitia michakato yao wenyewe halali wanapotumia hekima waliyojikusanyia katika kuangalia namna bora ya kutimiza malengo yao katika jiji husika. Kama jumuiya za imani katika Kristo, harakati za makanisa ya mijini lazima zihimizwe kufanya mazungumzo kuhusu miundo na taratibu zao za huduma ili kugundua njia bora zaidi za kuzingatia muktadha wa maeneo husika katika kueneza Injili na kuendeleza Ufalme wa Mungu kwa majirani zao.

Made with FlippingBook Digital Publishing Software