Theolojia Katika Picha

3 8 /

R e p r e s e n t a n d o l a t e o l o g í a

Funguo kwa Utafsiri wa Biblia (muendelezo)

B. Ni kwa namna gani kifungu hiki cha Maandiko ni “habari njema” Kwangu na kwa wengine? • Kwa namna gani kinamfunua Yesu na ufalme wake ujao? • Kwa namna gani kinahusiana na mpango mkuu wa Mungu wa ukombozi? C. Ni kwa namna gani kujua kweli kutoka kwenye kifungu hiki cha Maandiko: Kuna athiri mahusiano yangu na Mungu? • Jaribu kutambua ni kwa namna gani kanuni na mifano kutoka katika Maandiko haya vinakusaidia wewe kumpenda Mungu na kumtii kwa ukamilifu zaidi. Kuna saidia mahusiano yangu na wengine? • Hii inahusisha familia ya Kanisa, familia yangu binafsi, wafanyakazi wenzangu, marafiki zangu, majirani zangu, maadui zangu, wageni na maskini au wale wanaoonewa. Kuna nipa changamoto kwa yale ninayo yaamini, mtazamo wangu na matendo ambayo utamaduni wangu unaona ni kawaida? • Ni kwa namna gani namna ya kufikiri kwangu na kutenda kwangu lazima kuwe tofauti na wale walio katika ulimwengu unaonizunguka? D. Kuna jaribu kujibu maswali “natakiwa niamini nini?” Na “natakiwa kufanya nini?” Kwa sasa baada ya kuwa nimejifunza kifungu hiki cha Maandiko. • Je nahitaji kugeuka kutoka katika namna yangu ya kwanza ya kufikiri na kutenda? • Naweza kutendaje juu ya kweli hii ili niwe mtu mwenye busara?

E. Nawezaje kushirikisha wengine kile nilichojifunza kwa njia ambayo itavuta umakini wao kwa Kristo na kuwajenga?

Made with FlippingBook Digital Publishing Software