Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi

1 1 2 /

U O N G O F U & W I T O

6. Inamaanisha nini kusema kwamba Mungu ametuita tuishi kama watumishi wa kujidhabihu kwa utukufu wake? 7. Toa mfano unaoakisi maana ya “kufa kwa nafsi yako” ili kuishi kwa ajili ya Kristo. Je, kuishi kama watumwa wa Yesu kunamaanisha kwamba hatuwezi au hatupaswi kamwe kuwa watu “tajiri na mashuhuri”? Elezea jibu lako. 8. Fafanua usemi kwamba “ikiwa tunaishi au tukifa, sisi ni wa Bwana.” Je, mtu ambaye amekufa kwa nafsi yake na kujitoa kwa Mungu kwa ajili ya utukufu wake ni mtu mwenye mtazamo wa aina gani?

Neno Linaloita Sehemu ya 2

Mchungaji Dkt. Don L. Davis

Neno lililotugeuza na kutuita kwenye ufuasi, pia linatuita kuishi na kufanya kazi katika jumuiya, kama washirika wa familia yake tukufu, watu wa Mungu ( laos ). Kama washirika wa watu wa Mungu, tumeitwa kwenye uhuru, kutumia uhuru wetu katika Yesu Kristo kama fursa ya kutimiza Amri Kuu, yaani, kuwapenda na kuwatumikia wengine, na pia kwa kusudi la kuwaokoa wengine kwa ajili ya kudusi la Kristo. Kama washirika wa familia ya Mungu, wale walioitwa kwenye ufuasi, jumuiya, na uhuru, tumeitwa pia kushiriki katika utume wa Ufalme. Mungu Baba ametuita kutimiza Agizo Kuu, kupigana vita na adui yetu wa kiroho Ibilisi, na kuakisi maisha ya Ufalme kupitia upendo na matendo yetu mema. Lengo letu la sehemu hii ya pili ya Neno Linaloita ni kukuwezesha kuona kwamba: • Neno lile lile linalotuita sisi kuishi kama wanafunzi wa Yesu kibinafsi pia linatuita sisi kuishi na kufanya kazi katika jumuiya, kama washirika wa familia yake tukufu, watu wa Mungu ( laos ). • Kama washirika wa familia ya Mungu, tumeitwa kuishi maisha ya huru katika Yesu Kristo, na kutumia uhuru wetu katika Kristo kama fursa ya kuwapenda wengine, hivyo kutimiza Amri Kuu, na pia kutafuta kuwaokoa wengine kwa ajili ya Kristo.

Muhtasari wa Sehemu ya 2

4

Made with FlippingBook flipbook maker